MKUU WA WILAYA YA MPANDA AINGILIA KATI MGOGORO WA TENDA YA WAJASILIAMALI KUHUSU UTENGENEZAJI WA MADAWATI.


Na.Issack Gerald-Katavi
Umoja wa wajasiliamali Pasifiki waliopo mtaa wa majengo kata ya Kashaulili  umeilalamikia Manispaa ya Mpanda kwa kutoa tenda kwa mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Sailoni Mwagama ambaye ni mjasiliamali wa eneo hilo tofauti na ilivyokuwa awali kuwa wajasiliamali hao wangepata tenda hiyo kwa pamoja kama ilivyokuwa imetangazwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Bw.Pazza Mwamlima.

Kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mpanda,akitoa ufafanuzi wa malalamiko hayo katibu tarafa wa Tarafa ya kashauriri Bw. Reginard Muhango katika mkutano uliofanyika  eneo hilo, amesema lengo na hadi ya mkuu wa wilaya ni kutoa tenda kwa kila mwana pasifiki na si kwa mtu mmoja.
Wakati Bw. Mhango akiwatoa wasiwasi wajasiliamali hao pia aliwaahidi kuwa huo siyo mwisho wa tenda kufika mahali hapo.
Hata hivyo alimuamru mwenyekiti wa eneo hilo,kugawa magogo kwa kila mjasiliamali ili kutengeneza madawati hayo.
Aidha ametoa wito kwa wajasiliamali hao kuendelea na kazi kama kawaida pamoja na kudumisha umoja kati yao na kuchangamkia fursa wanazopata ili kutengeneza vitu vyenye ubora na ustadi wa hali ya juu.
Tenda ya utengenezaji wa madawati kwa ajili ya Shule Wilayani Mpanda ilitangazwa na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda mnamo Februari 27 mwaka huu ambapo zaidi ya Magogo 130 yalitakiwa kugawanywa kwa wajasiliamali hao zaidi ya 300 badala yake kuchukuliwa na mtu mmoja hali ambayo ndiyo imesababisha hali ya kutoelewana kwa wajasiliamali wenyewe na hatimaye Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kulalamikiwa.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA