MKOA WA KATAVI WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA ARDHI.


Na.Issack Gerald-Katavi
MKOA wa Katavi umeshauriwa kumaliza migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji na katika maeneo ya makazi na hifadhi.
Ushauri huo umetolewa jana na Waziri mkuu mstaafu Mh, Mizengo Pinda katika kikao cha Kamati ya ushauri ya mkoa kilichofanyika katika ukumbi wa idara ya maji mjini Mpanda.

Amesema migogoro ya ardhi inasababishwa na ongezeko la watu wanaohamia ndani ya mkoa wa Katavi kutoka mikoa mingine nchini bila kufuata maelekezo ya waraka wa serikali wa mwaka 2000.
Waziri mkuu mstaafu Pianda ameshauri mjadala huo upewe nafasi kubwa na kila halmashauri mkoani Katavi itoe mwongozo wa matumizi ya ardhi na kutoa taarifa katika ngazi ya mkoa ili ufumbuzi wa tatizo hilo uweze kupatikana.
Kikao hicho kimeshirikisha wadau mbali mbali wa maendeleo mkoani Katavi wakiwemo wabunge saba wakiwemo watano wanaochaguliwa na wananchi.
Migogoro mingi katika Mkoa wa Katavi imekuwa ikiibuka ikihusisha wakulima na wafugaji,maafisa kuuza kiwanja kwa mtu zaidi ya mmoja,wakulima kuingia katika eneo la hifadhi za mkoa wa Katavi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA