UTAPELI WA FEDHA ZA WALIMU KWA MTANDAO WAENDELEA KULINDIMA KATAVI,C.W.T KATAVI YAWATAHADHARISHA WANACHAMA WAKE


Na.Issack Gerald-Mpanda
Chama cha walimu Tanzania (C.W.T) Mkoani Katavi,kimetoa tahadhari kwa wanachama wa chama hicho na watumishi wengine kuwa makini kutokana na utapeli kwa kimtandao ambao umejitokeza ukifanywa na watu wasiofahamika.

Tahadhari hiyo imetolewa na leo na Mwenyekiti wa C.W.T Mkoani Katavi Mwalimu Gerigori John Mshota wakati akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA sambamba na Mpanda Radio Fm Ofisini kwake.
Amesema kuwa kumezuka makundi ya watu wanaojitambulisha kuwa ni Viongozi wa C.W.T  kikanda wakiwataka walimu wawape namba za akaunti za benki ili walipwe mishahara yao.
Aidha amesema kuwa Takribani watu wanne wakiwemo walimu walitapeliwa  milioni kadhaa na watu wasiowafahamu kwa kutumia mitandao ya mawasiliano.
Kati ya walimu wawili ambao wamepokea mawasiliano kutoka kwa matapeli mwezi Februari mwaka huu wakiwa katika harakati za kutapelewa yumo mmoja wa Shule ya Sekondari Mwangaza iliyopo Manispaa ya Mpanda.
Amesema kuwa amekuwa akijitambulisha kuwa yeye ni mlezi wa chama cha Walimu Tanzania C.W.T katika mikoa ya Rukwa,Katavi na Kigoma.
Kwa upande mwingine chama kimeliomba jeshi la polisi kusaidia kuwakamata watu wanaojihusisha katika wizi wa kutumia mitandao.
 Mwaka jana mbali na walimu kudai kutapeliwa wengi wa wananchi walisema kuwa walitapeliwa fedha zao ambapo wimbi hilo limeendelea kuwakumba waliowengi.
Katika hatua nyingine mwenyekiti wa C.W.T amewataka walimu waliokuwa wakifanya kazi kwa mkataba kutoka yaliyokuwa makazi ya wakimbizi na sasa makazi mapya,kuwa wavumilivu wakati madai yao ya kupatindishwa madaraja na stahiki nyingine zikiendelea kufanyiwa kazi na mamlaka husika.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA