KUJENGWA MAHAKAMA KATIKA MAKAZI MAPYA YA KATUMBA NA MISHAMO KATAVI KWAPUNGUZA UHARIFU


Na.Issack Gerald-Mpanda
Kujengwa kwa mahakama ya mwanzo katika eneo la makazi ya Mishamo na Katumba kumepunguza kiwango cha uharifu ambao umekuwa ujitokeza katika makazi hayo.

Hayo yalibainishwa jana na Wakili wa UNHCR Adolf Mishanga ambaye ni mkuu wa Ofisi ya UNHCR Mishamo kwa niaba ya Mkuu wa Ofisi ya UNHCR Wilayani Mpanda katika maadhimisho ya siku ya Sheria duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Mahakama ya Wilaya.
Licha ya kutotaja takwimu ya uharifu katika makazi hayo Bw.Mishanga pia ameiomba idara ya Mahakama  kujenga mahakama ya Wilaya katika makazi hayo ili kurahisha huduma mbalimbali kwa wakazi waliopo katika maeneo hayo.
Wakati huo huo Bw.Misanga alisema kuwa idadi ya wakimbizi dunia Nzima imefikia milioni 60 huku Mkoani Katavi idadi ya wakimbizi ikipungua baada ya Tanzania Kutoa uraia kwa waliokuwa wakimbizi.
Aidha katika kuhakikisha shughuli za mahakama zinatekelezeka katika kiwango kinachotakiwa,Shirika la Wakimbizi duniani UNHCR limesema kuwa litaendelea kushirikiana na mahakama Mkoani Katavi na Tanzania kwa ujumla ambapo katika maadhimisho ya siku ya sheria yaliyofanyika jana shirika hilo limetoa nakala 620 vyenye sheria mbalimbali ili kutafsiri  sheria  namna ya kuhudumia wakimbizi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA