WANAWAKE WAISHI KWA MIGOGORO KATIKA NDOA KISA UCHAGUZI OKTOBA 25,2015


Na.Issack Gerald-Mpanda
BAADHI ya wanawake Mkoani Katavi wameiomba Serikali na wadau mbalimbali kuelimisha  jamii kwa chaguzi zijazo ili kukomesha tabia ya ukandamizaji unaofanywa na baadhi ya wanaume kwa kuwachagulia vyama vya siasa wake zao.
                                                        
Baadhi ya wanawake ambao wamezungumza na P5 TANZANIA(Picha na Issack Gerald)

Wakizungumza na P5 TANZANIA MEDIA wamesema, katika kipindi cha uchaguzi wa mwaka 2015, walikabiliwa na changamoto za kuchaguliwa vyama na waume zao pamoja na lugha za matusi kwa baadhi ya vijana ambao waliwataka kuwa chama kimoja.
Wamesema mpaka sasa baadhi ya wanawake wameachika na wengine kuishi katika migogoro ya ndoa pamoja na chuki kati yao na baadhi ya vijana kutokana na tofauti za itikadi ya vyama vya siasa.
Pamoja na changamoto walizozipata wanawake hao pia wamepongeza uchaguzi huo kufanyika kwa amani na utulivu.
Aidh awamesema kuwa kutolewa kwa elimu ya uchaguzi kwa jamii kuwatambua wanawake kuwa wana uwezo wa kuongoza kutatoa fursa ya kuongeza idadi ya wanawake katika ngazi mbalimbali za maamuzi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA