HALMASHAURI ZA WILAYA KATAVI ZATAKIWA KUTATU CHANGAMOTO YA MIUNDOMBINU YA ELIMU KUFANIKISHA BRN


Na.Issack Gerald-MPANDA
HALMASHAURI zote zilizomo ndani ya mkoa wa katavi zimetakiwa kufanya jitihada za kutatua  changamoto za miundombinu ya elimu ili kuhakikisha wanafunzi wote wanasoma vizuri.

Hayo yamesemwa na Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Katavi Bw.Said Mwapongo  wakati akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA ofisini kwake kwa njia ya simu.
 Amesema tayari ngazi ya mkoa imekutana na ngazi za halmashauri lengo likiwa ni kuangalia utatuzi wa changamoto  hizo kutokana na ongezeko la wanafunzi katika sule mbalimbali.
Aidha  Bw mwapongo ameitaka jamii kuwapeleka watoto shule bila kisigizio  chochote cha kutokuwa na sare ya shule  na kuwa kwa mzazi au mlezi atakosa sare ya shule ampeleke  atapokelewa huku jitihada za kutafuta sare zikiendelea kufanyika.
Mkoa wa Katavi unaundwa na Halmshauri 5 ambazo ni Halmshauri ya Wilaya ya Mpanda,Halmshauri ya Manispaa ya Mpanda,Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo,Halmshauri ya Wilaya ya Mlele na Halmshauri ya Wilaya ya Mpimbwe

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA