AFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA KWA TUHUMA ZA UHARIBIFU WA MALI,YUMO PIA ALIYETISHIA KUUWA KWA MANENO


Na.Boniface Mpagape-Mpanda
MTU mmoja mkazi wa Kapalangeo-kazima katika manispaa ya Mpanda Bw. Joseph Saleh kajunja amefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda akikabiliwa na shtaka la kuharibu mali.

Akisomewa shtaka mbele ya hakimu Robert Nyando, mshtakiwa alitenda kosa hilo tarehe 26 mwezi huu katika eneo la soko kuu Mpanda mjini kwa kuvunja kioo cha bajaji yenye namba za usajili T 810 AGF chenye thamani ya shilingi laki moja na elfu themanini, mali ya Bw. Dalam Moshi. Mshtakiwa amekana shraka hilo.
Hakimu wa mahakama hiyo Bw. Robert Nyando, amesema mshtakiwa ana haki ya kupata dhamana ya ahadi ya shilingi laki mbili na elfu hamsini na mdhamini awe na barua toka kwa mtendaji wa kijiji na kitambulisho.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 8 mwezi Februari mwaka huu itakaposikilizwa.
Wakati huo huo, miongoni mwa kesi zilizotajwa leo ni ya kutishia kuua kwa maneno ambapo Mlalamikaji Bi. Agnes Elikana amefikisha shtaka hilo katika mahakama ya mwanzo Mjini Mpanda, kwa kutishiwa kuuliwa kwa maneno na Maria Joseph mkazi wa Kilimahewa.
Imeelezwa mahakamani hapo kuwa mshtakiwa Maria joseph alitenda kosa hilo tarehe 12 mwezi huu majira ya saa 11 jioni huko Kilimahewa kata ya Shanwe, kwa kumtishia Agnes Elikana kwamba atampiga mpaka amuue.
Baada ya kusomewa shtaka mshtakiwa amekana kosa na hakimu wa mahakama hiyo aliyesikiliza kesi hiyo Bw. Sylivester makombe amesema dhamana ipo wazi kwa mshtakiwa ya ahadi ya shilingi laki mbili na awe na kitambulisho. Mshtakiwa amedhaminiwa na kesi hiyo itasikilizwa tarehe 05 mwezi Februari mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA