WANAWAKE MPANDA NDOGO NA KABUNGU WAONGOZA KWA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI


Na.Issack Gerald-MPANDA
Jumla ya watu 14 kati ya 169 waliopima Virusi vya Ukimwi Mwezi Novemba mwaka huu katika Kata ya Kabungu na Mpanda Ndogo wamegundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Hayo yamebainishwa  na Bahati Mwailafu Afisa ustawi wa Jamii ambaye pia ni Kaimu Mratibu wa Ukimwi Halmshauri ya Wilaya ya Mpanda,wakati akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA Ofisini kwake kuhusu mikakati ya Halmashauri kupamba na Ugonjwa wa Ukimwi.
Aidha Mwawilafu amesema kuwa Halmshauri itaendelea kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Ukimwi katika kata zote 16 za Halmashauri hiyo.
Katika takwimu za maambukizi ya Virusi vya Ukimwi ambazo zimeapatikana kwa kipindi cha mwezi Novemba mwaka huu toafauti na takwimu ambayo imekuwepo katika kata mbili kati ya 16 inaonesha kuwa kata ya  Kabungu jumla ya waliopima virusi vya Ukimwi  ni 117,Walioatharika-8 kati yao Wanawake-6 na Wanaume-2 huku Kata ya Mpanda ndogo Walioapima wako 52,Wanawake-43 na Wanaume-09 ambapo  wathirika ni mwanaume 1 na wanawake -5
 Mkurugenzi wa Taasisi ya Kiraia ya UDESO Eden Ezekiel taasisi ambayo makao makuu yako Usevya katika Wilaya ya Mlele ametoa shukrani kwa wafadhiri mbalimbali wakiwemo watu wa Marekani wanaochangia nguvu kubwa kupambana na virusi vya Ukimwi na kuishauri serikali kuwekeza bajeti kubwa katika mapambano ya Ukimwi .
Hata hivyo wakazi wote Mkoani Katavi wametakiwa kutumia elimu wanayopewa kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.
Mkoa wa Katavi una asilimia 5.9 ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi katika utafiti uliofanyika miaka ya hivi karibuni.
Siku ya Ukimwi duniani huadhimishwa Desemba Mosi ya Kila mwaka.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA