WAKAZI MPANDA WACHARUKA KUANDIKIWA RISITI TOFAUTI NA PESA WANAYOLIPA KWA USHURU WA KUZOA TAKA



Na.Issack Gerald-MPANDA
BAADHI ya wakazi wa mtaa wa Mpanda Hotel  C Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,wamelalamikia hatua ya kupewa lisiti iliyoandikwa fedha tofauti na kiasi wanacholipa kwa ajili ya kuzoa taka katika mtaa huo.

Wakizungumza na P5 TANZANIA MEDIA wamesema wamekuwa wakipewa lisiti zilizoandikwa shilingi mia tano badala ya shilingi elfu moja wanayolipa kama utaratibu wa Manispaa unavyoelekeza.
Wakazi hao wameitaka  Halmshauri ya Manispaa ya Mpanda kuweka nafasi ya kuandika jina la mchangiaji wa mchango wa ushuru katika lisiti tofauti na ilivyo sasa ambapo listi hiyo haioneshi jina la mchangiaji.
Hata hivyo mjumbe wa mtaa wa Mpanda Hotel C Leonard Sokoni  aliyehusika kutoa lisiti hizo, amekiri kukiuka utaratibu wa utoaji lisiti hizo na ameahidi kurudia kutoa lisiti nyingine kama utaratibu unavyoelekeza.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA