MKURUGENZI MKUU RAHCO ASIMAMISHWA KAZI


Na.OFISI YA MAWASILIANO YA IKULU.
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk.John Magufuli amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli Tanzania (RAHCO), Benhadard Tito.
                                               
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli

Rais Magufuli amesema,amemsimamisha Bw. Tito kupisha uchunguzi wa kina kutokana na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za manunuzi, yaliobainika katika mchakato wa utoaji wa zabuni ya ujenzi wa Reli ya Kati.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, Dk Magufuli,amefikia uamuzi huo baada ya kuitisha kikao cha wataalamu kutoka wizara na taasisi mbalimbali za serikali, ambazo zinahusika katika utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha kisasa.
Aidha Rais Magufuli ameivunja Bodi ya Rahco baada ya kujiridhisha kuwa haikutekeleza ipasavyo wajibu wake katika kusimamia mchakato wa zabuni hiyo na badala yake imeonekana kutetea kilichofanyika.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA