BAADHI YA WAMILIKI WA VITUO TIBA ASILIA NA TIBA MBADALA MPANDA WAZUNGUMZIA ZUIO LA SERIKALI KUWEKA MATANGAZO REDIONI


Na.Issack Gerald-MPANDA
Baadhi ya wamiliki wa vituo vya tiba asilia na Tiba Mbadala Wilayani Mpanda Mkoani Katavi wamesema kuwa Serikali Ya Tanzania haijakosea kusitisha utangazaji wa vituo hivyo katika vyombo vya habari kwa kuwa serikali imesimamia sheria za nchi.
                                                     
ALOVERA Miongoni mwa mimea inayotibu baadhi ya magonjwa
Hayo yamebainishwa na Wamiliki hao kwa nyakati tofauti, wakati wakizungumza na P5 TANZANIA MEDIA katika Ofisi zao mara baada ya tangazo la serikali.
Miononi mwa wamiliki wa vituo vya tiba mbadala na tiba asilia ni pamoja na Bw.Joseph Kienzi ambaye ni mmiliki wa kituo cha Jerusalem Herbalist Clinic kilichopo Mjini Mpanda ambaye amewashauri wamiliki wa vituo kama hivyo kuhakikisha wanapata kibali kutoka Wizara ili kufanya kazi kwa uhuru.
Kwa Mjibu wa Bw.Joseph amesema kuwa,vibali vya kutangaza matangazo katika vyombo vy ahabari vimekuwa vikitolewa na Ofisi za usitawi wa jamii katika Halmashauri za wilayakatika mikoa husika ambapo amesema kuwa kwa sasa wamiliki wa vituo hivyo wanatakiwa kupata kibali kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
Tangazo la serikali kupiga marufuku utangazaji wa matangazo ya tiba asilia na tiba mbadala katika vyomvo vya habari lilitangazwa Ijuma iliyopita.
Katika hatua nyingine wamesema kuwa,mpango huo wa serikali utawabana matapeli wa tiba mbadala na tiba asilia ambao wamekuwa wakiwatapeli wananchi kwa kuwaibia pesa wakisema kuwa wanawatibu huku wakiwa hawana kibali cha kufanya matibabu hayo.
Hata hivyo serikali ilitoa siku 14 kwa wamiliki wa vituo vya Tiba Mbadala na tiba asilia wawe wamewasilisha Wizarani nyaraka za kazi zao ili kupata vibali halali.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA