MWANAUME MMOJA AKUTWA AKIWA AMEKUFA WILAYANI MLELE


Issack Gerald-KATAVI
MTU Mmoja jinsia ya Kiume ambae hakutambulika jina wala umri wake ameuwawa  kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali katika kijiji cha tumaini kata ya Itenka Wilayani Mlele.

Taarifa ya Jeshi la polisi kwa vyombo vya habari imesema tukio hilo limetokea Usiku wa kuamkia juzi ambapo mwili wa marehemu ulichomwa moto na watu wasiojulikana baada ya kutekeleza Mauaji hayo.
Katika tukio linguine mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Obed Yoram (35) Muha Mkazi wa Kijiji cha Vikonge Kata ya Mpanda ndogo wilayani Mpanda ameuwawa kwa kupigwa na fimbo na kasha mwili wake kuchomwa moto.
Kufuatia Matukio hayo Jeshi la polisi Mkoani hapa linaendelea na Msako ili kuwabaini watuhumiwa wa Makosa mbalimbali ili wafikishwe katika vyombo vya sheria.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA