VIONGOZI WA UMMA TANZANIA WATAKIWA KUWA WAZALENDO KUPITIA WANAOWAONGOZA


 Na.Issack Gerald-KATAVI

Viongozi wa umma hapa nchini wametakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia Uzalendokatika kutekeleza mahitaji ya wanaowaongozana siyo kwa maslahi binafsi.

Wito huo umetolewa leo na wajumbe wa semina ya utawala bora wa rasilimali asilia inayofanyika katika manispaa ya Mpanda.
Wamesema kuwa miradi mingi ya maendeleo imekuwa haitekelezeki kwa wakati katika maeneo mengi hapa nchini, kutokana na watawala kutoa kipaumbele katika masuala binafsi kwa kutumia rasimaliza taifa na kusahau kuwapa wananchi mahitaji ya msingi.
Semina hiyo inayofanyika kwa usimamizi wa taasisi ya Jane Goodall inayojishughulisha na uhifadhi wa mazingira, na kuhudhuriwa na wadau wa mazingira kutoka wilaya za Mpanda, Nsimbo, Uvinza na Kigoma, inatarajiwa kukamilika ijumaa wiki hii.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA