IGP MANGU AHIMIZA AMANI KATAVI


NA.Issack Gerald-Katavi
MKUU wa jeshi la polisi nchini Inspekta jenerali Ernest Mangu, amesema kila mtu atimize wajibu wake ili kuhakikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu, unafanyika kwa amani na utulivu.

IGP Mangu ametoa kauli hiyo juzi katika hoteli ya Lyamba Lya Mfipa mjini Mpanda, wakati akizungumza na wadau mbali mbali wa jeshi la polisi wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa na jeshi la polisi.
Awali Mkuu wa mkoa wa Katavi Dk. Ibrahim Msengi alimueleza Mkuu wa jeshi la polisi nchini kuwa hali ya usalama mkoani Katavi ni shwari kutokana na kazi nzuri inayofanywa na kamati ya usalama ya mkoa, na kuwataka wakazi wa mkoa wa katavi kuendeleza amani iliyopo.
Hafla hiyo imehudhuriwa na wadau mbali mbali, wakimwemo viongozi wa dini, mashirika yasiyo ya kiserikali, taasisi za fedha, wafanyabiashara, pamoja na waandishi wa habari.


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA