AFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA KWA TUHUMA ZA UHARIBIFU WA MALI NA KUTELEKEZA FAMILIA.


Na.Issack Gerald-MPANDA
Mtu mmoja mkazi wa mtaa wa Kasimba manispaa ya Mpanda jana amefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda akikabiliwa na shtaka la kuharibu mali na kutelekeza familia.

Hakimu wa mahakama ya mwanzo mjini Mpanda Bw. David Mbembela amemtaja mshtakiwa kuwa ni Juma Balison mwenye umri wa miaka 27, na kwamba alitenda kosa hilo tarehe 30 mwezi desemba mwaka 2015.
Amemtaja mlalamikaji katika kesi hiyo kuwa ni Magreth Joseph, na inadaiwa kuwa mshtakiwa aliharibu vyombo vya ndani ambavyo ni ndoo sita za plastiki na masufuria manne kwa kuviponda ponda kwa nyundo.
Inadaiwa pia kuwa mshtakiwa alikataa kutunza watoto aliozaa na mlalamikaji Bi. Magreth Joseph. Hata hivyo, mshtakiwa Juma Balison amekana shtaka hilo na kesi hiyo imeahirishwa na itatajwa tena tarehe 17 mwezi huu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA