Posts

MSITU WA TONGWE MAGHARIBI WENYE SOKWE ZAIDI YA 800 SASA MIKONONI MWA HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA

Image
Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mbwana Muhando akizungumza na wananchi wa kijiji cha Katuma(PICHA NA Issack Gerald) Sokwe moja ya wanyama wanaopatikana msitu wa Tongwe Magharibi Baadhi ya wananchi katika kijiji cha Kapanga wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Mpanda Salehe Muhando(Hayupo pichani)(PICHA NA Issack Gerald) Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi Salehe Muhando,amesema wizara ya maliasili na utalii imekubali msitu wa Tongwe Magharibi kumilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda kutoka katika mamlaka ya wizara hiyo. Muhando amebainisha hatua hiyo kupitia mikutano ya hadhara katika vijiji vya Kapanga na Katuma Kata ya Katuma lengo likiwa ni kuelimisha kutunza msitu huo wenye zaidi ya sokwe 800 kwa ajili ya faida ya vizazi vya sasa na vijavyo.

RAIS MAGUFULI ASIKITISHWA NA KIFO CHA MARIA NA CONSOLATA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli ameungana na Watanzania kuomboleza msiba wa watoto Maria na Consolata,waliofariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya mkoa wa Iringa. Rais Magufuli katika ukurasa wake wa Twitter ametuma ujumbe akielezea kusikitishwa kwake na msiba wa watoto hao ambao hivi karibuni aliwatembelea walipokuwa hospitali ya Muhimbili wakipatiwa matibabu hivi karibuni. Vifo hivyo vimetokea siku chache baada ya kuruhusiwa kutoka Hospotali ya Taifa Muhimbili ambako walikuwapo zaidi ya miezi miwili wakipatiwa matibabu. Taarifa kutoka Hospitali mkoani Iringa zinaeleza kuwa watoto hao walifariki kwa muda tofauti ambapo mmoja alifariki saa 1 usiku na mwengine alifariki saa 3 usiku. Maria na Consolata ambao ni pacha walizaliwa hapa nchini wakiwa wameungana na wakaishi hadi kujiunga na chuo kikuu wakiwa bado wameungana. Pacha hao waliokuwa na umri wa miaka 22 wamekuwa wakitunzwa na watawa wa kanisa Katoliki tangu na baada ya kuza...

ASASI ZA KIRAIA ZAINGILIA KATI SUALA LA KUONDOLEWA WALIMU WA ELIMU MAALUMU SHULENI AZIMIO

Image
Asasi za kiraia Mkoani Katavi zimelazimika kufika katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi ili kuzungumza naye kuhusu hatua ya kuwaondoa walimu waliokuwa wakifundisha watoto wenye ulemavu katika Shule ya Msingi Azimio bila kuweka wengine mbadala. Asasi hizo zimesema katika kipindi cha mwaka 2015 mpaka sasa wanafunzi wenye ulemavu hawafundishwi masomo inavyotakiwa baada ya walimu watatu kati ya watano wa elimu maalumu waliokuwepo kuondolewa katika shule hiyo na kupangiwa majukumu mengine. Zimesema,walimu watatu walioondolewa shuleni walipandishwa madaraja kuwa walimu wakuu katika shule zisizokuwa na watoto wenye ulemavu,mwingine akipandishwa daraja na kuwa mratibu elimu maalumu katika Manispaa ya Mpanda ambapo mpaka sasa amebaki mwalimu mmoja anayefundisha darasa la kwanza mpaka la saba. Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Bw.Michael Nzyungu amesema hakuwa na taarifa ya kuondolewa kwa walimu hao...

NKASI KINARA WA MIMBA KWA WANAFUNZI MKOANI RUKWA

Afisa serikali za mitaa mkoani Rukwa Bw.Albinus Mgonya amesema halmashauri ya wilaya ya Nkasi mkoani humo ndiyo inayoongoza kwa wanafunzi kupata ujauzito mkoani Rukwa. Mgonya amebainisha hali hiyo kupitia kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika juzi katika halmashauri hiyo. Katika kipindi cha miezi tisa jumla ya wanafunzi 74 wamekatiza masomo kutokana na kupata ujauzito ambapo kwa mjibu wa katika takwimu hiyo,wanafunzi 36 ni wanafunzi wa shule za msingi na wanafunzi 38 wa sekondari waliopata ujauzito huo kuanzia Julai mwaka jana mpaka Aprili mwaka huu. Alisema kulingana na takwimu hizo,wanafunzi wanaopata ujauzito ni sawa na kuwa kila mwezi wanafunzi   wanne wa shule za msingi   wanapata ujauzito sambamba na wanne wa sekondari wanapata ujauzito. Kutokana na hali hiyo,Mgonya ameiagiza halmashauri ya wilaya Nkasi kuandaa taarifa itakayoainisha idadi ya Watoto wenye mimba,mahali walipo wazazi   wao ikiwa ni pamoja na viongozi wa maeneo yao hasa Watendaji wao wa ...

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

Image
Abdulrahman Kinana alizaliwa mwaka 1952 mkoani Arusha Arusha Kaskazini mwa Tanzania. Kinana ni mwanasiasa aliyeshika nyadhifa mbalimbali serikalini. Alihitimu shahada yake katika Chuo Kikuu cha Havard nchini Marekani akibobea kwenye masuala ya mikakati. Alikuwa Waziri wa ulinzi na Jeshi la kujenga taifa ,naibu Waziri wa mambo ya nje na uhusiano wa kimatafa na Waziri wa ulinzi. Kinana aliwahi kufanya kazi na Jeshi la wananchi la Tanzania kwa miaka 20 kabla ya kusaafu akiwa na cheo cha ukanali mwaka 1972. Abdulrahman Kinana pia aliwahi kuwa Spika wa Bunge la Afrika mashariki mwaka 2001 mpaka mwaka 2006. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

WAKAZI WILAYANI TANGANYIKA WATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI YA UGONJWA WA KIPINDUPINDU

Kaimu   Afisa wa Afya wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi Bw.Philipo Mihayo amewataka wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya ugojwa wa kipindupindu kwa kufanya usafi wa   chakula na mazingira yote yanayowazunguka. Bw.Mihayo amesema ni vema   kuchukua tahadhari kwani mikoa jirani ya Rukwa na kigoma inaripotiwa kukubwa kadhia hiyo. Aidha Mihayo ametoa wito kwa wananchi kuchimba vyoo vya kisasa lakini pia kuhakikisha wanatumia maji safi na salama huku wanaokadi maelekezo akisema watachukuliwa hatua. Wilaya jirani ya Sumbawanga iliyopo Mkoani Rukwa ilitangaza kuwa katika kipindi cha Mei 11 mpaka 24 watu 7 walikuwa wamefariki dunia huku wengine 166 wakiugua ugonjwa wa kipindupindu na 44 mpaka kufikia Mei 25 walikuwa wakiendelea kupatiwa matibabu. Kipindupindu husababishwa na bakteria aina ya  Vibrio cholerae  zinazosababisha kuhara majimaji yenye rangi kama maji ya kupikia  mchele ambapo bakteria hao walitambuliwa mwaka  1854  . Habari zaid...

BARABARA YA MPANDA-TABORA SASA RUKSA KWA MAGARI YOTE

Mkuu wa mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Mhuga hatimaye ametangaza rasmi kuwa magari yote makubwa kwa madogo yanaruhusiwa kusafiri kwa kutumia barabara ya Mpanda --Tabora kupitia Mto Koga wilayani Mlele Mei 30,2018. Kwa mjibu wa Bw.Aman   Mwakalebela ambaye ni Afisa Mfawidhi wa mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa majini na nchi kavu SUMTRA amesema hali ya barabara hiyo ni nzuri na inaruhusu magari ya aina zote kupita. Hata hivyo Mwakalebela amewataka abiria waliotoa nauli ya mzunguko wa barabara kupitia Kigoma au Mbeya kwa ajili ya kwenda Tabora kudai kurejeshewa kiasi cha   nauli iliyozidi kiwango cha fedha kutoka Mpanda-Tabora na kusafiri kwa gharama halisi. Mei 26 mwaka huu Mkuu wa mkoa wa katavi Meja Jenerali Mstaafu Rapahael Muhuga alitangaza kuruhusu magari yasiyozidi tani 3 huku ukarabati wa barabara hiyo ukiendelea. Aprili 14 mwaka huu,Muhuga alitanagaza kuifunga barabara hiyo kutokana na kujaa maji katika daraja la mto koga hali iliyokuwa ikihatar...