Posts

MAKAMU WA RAIS AFUNGIWA MAISHA

Image
Makamu wa Rais wa shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania (TFF),Michael Wambura amefungiwa kifungo cha maisha cha kutojihusisha na mchezo wa soka popote pale. Michael Wambura Jana mchana afisa habari wa TFF Clifford Mario Ndimbo aliwaambia waandishi wa habari kuwa Wambura amefanya makosa hayo huku akijua anashusha hadhi ya shirikisho hilo ikiwa ni kinyume na katiba ya TFF. Ndimbo alisema  Wambura alikuwa na uhuru wa kufika mwenyewe mbele ya kamati na kutoa utetezi wake kwa njia mdomo,kutuma kwa maandishi au kupeleka mashahidi au kutuma mwakilishi ambaye ataambatana na barua ya uwakilishi ambapo Wambura alituma mwakilishi ambaye ni Wakili Emanuel Muga kwa ajili ya kumtetea. Alisema kamati hiyo iliyokaa jana ikiongozwa na Mwenyekiti wake Hamidu Ally Mbwezereni,wamemkuta na makosa matatu yatakayomfanya Wambura asijihusishe na masuala ya soka. Kosa la kwanza amevunja kifungu no 73 kwa kupokea malipo yasiyo halali ya TFF, ambapo faini yake ni milioni 10, kutojihusisha na sok...

RAIS MAGUFULI AAGIZA WAFANYABIASHARA WADOGO WA STENDI MOROGORO WASIBUGHUDHIWE

Image
Mwanamke aliyejitambulisha kwa jina   moja la Avintishi,leo amejitoa kimasomaso na kumueleza Rais John Magufuli kuhusu kero wanayopata wafanyabiashara ndogondogo ikiwamo kunyang’anywa bidhaa zao. Mwanamke huyo ametoa kero hiyo leo,katika uzinduzi wa kiwanda cha Sigara cha Philip Morris mkoani Morogoro. Baada ya kueleza hayo,Rais alimuita Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro,John Mugarula kujibu kero zilizoibuliwa na mama huyo ambapo Mkurugenzi huyo, alisema wanawaondoa wafanyabiashara hao kwa sababu wametengewa maeneo maalumu huku akisema sababu ya suala la kipindupindu. Baada ya hapo Rais,alimuhoji mama huyo,ni kiasi gani alitozwa na askari mgambo wa manispaa,mama huyo akaeleza kuwa alitozwa Shilingi 200, 000. Rais alihoji tena,iwapo mama huyo anamkumbuka askari mgambo aliyemtoza kiasi hicho? Ambapo Baada ya kusema hayo,Rais alimpa mama huyo fedha na kumtaka mkurugenzi kumpa kiasi kingine cha fedha mama huyo. Kufuatia hatua hiyo,Rais aliagiza kuanzia leo,...

ACT-WAZALENDO WALAANI UHARIFU MKOANI KATAVI

Image
Viongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Mkoani Katavi, wamelaani matukio mbalimbali ya uharifu yanayoendelea kujitokeza Mkoani Katavi na kusababisha mauaji ya raia na wengine kadhaa kujeruhiwa. Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo John Malack pamoja na katibu wa chama hicho Bw.Joseph Mona wamevishauri vyombo vyote vya ulinzi na usalama kutafuta namna ya kudhibiti waharifu ili kuimarisha usalama wa raia ma mali zao. Kwa upande wao baadhi ya vijana Mkoani Katavi wamesema, ukosefu wa ajira kwa vijana wengi waliopo mitaani ni miongoni mwa vyanzo vinavyochangia kuongezeka kwa uharifu. Kuanzia mwezi Januari mpaka Machi mwaka huu,zaidi ya watu watatu wamefariki dunia katika matukio matatu tofauti yakiwemo matukio mawili ya ujambazi Januari 27 kata ya Ugalla,Februari 25 mwaka huu katika Mgodi wa dhahabu wa Isulamilomo wilayani Mpanda na lingine la Januari 22 likihusisha kifo cha mwanafunzi aliyeuwawa kikatiri wilayani Tanganyika. Habari zaidi ni P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

MWANAFUNZI AFARIKI MAZINGIRA YA KUTATANISHA POLISI WAWASHA TAA NYEKUNDU

Image
Jeshi la polisi mkoani Iringa linawashikilia watuhumiwa wawili kufuatia kifo cha kutatanisha cha mwanafunzi wa kike wa kidato cha sita Sundi George. Kwa mjibu wa Kamanda wa Polisi mkoani humo ACP Juma Bwire amesema mwanafunz huyo alikuwa akisoma katika shule ya sekondari Mwembetogwa.

WANANDOA WAFA MAJI

Image
Watu wawili ambao ni wanaondoa wamefariki dunia katika Wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha baada ya kuchukuliwa na mafuriko katika mto Piyaya Kata ya Piyaya wilayani humo. Picha hii haina uhusiano wowote na habari hii ni kuonesha picha maji tu Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Yusuph Ilembo amesema miili hiyo imeonekana leo majira ya asubuhi baada ya maji ya mto huo wa msimu kupungua.

RUKWA BADO WALIA NA UHABA WA VYUMBA VYA MADARASA

Image
MKOA wa Rukwa bado unakabiliwa na upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa ambapo jumla ya vyumba 4,226 vinakitajika ili  kumaliza tatizo hilo. Afisa elimu mkoa huo Nestory Mroka alisema mahitaji hayo yamekuwa yakisababisha mkoa huo kutopiga hatua katika mafanikio ya elimu. Alisema ili wanafunzi wafanye vizuri katika masomo yao ni lazima kuwe na miundombinu mizuri,walimu wa kutosha,vitabu pamoja na walimu lakini kama kuna mapungufu kati ya hayo mambo hata ufaulu hauwezi kuwa mzuri. Aidha Mroka alisema kutokana na changamoto hizo jitihada za makusudi zinahitajika katika kulimaliza tatizo hilo pamoja na mengine ili kuinua ufaulu wa wanufunzi katika shule za msingi pamoja na sekondari ambapo mpaka sasa ufaulu katika kidato cha nne ni wastani wa daraja la nne. Wakati huo huo,Afisa elimu huyo alisema yeye binafsi amejitahidi kuhakikisha anawasimamia walimu ili watimize wajibu wao ipasavyo ikiwamo kuwepo kazini kwa muda mwafaka sambamba na kufundisha kwa juhudi zote ili ida...

AUWAWA KWA SABABU YA MASHAMBA YAKE MJUKUU WAKE AHUSISHWA

Image
JESHI la Polisi mkoani  Rukwa,linawashikilia watu sita akiwemo mjukuu aliyekubalichukua hongo Shilingi milioni moja na kukubali babu yake auawe kwa kupigwa rungu kichwani kutokana na ugomvi wa ardhi. Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa,George Kyando alisema jana kuwa tukio la kuuawa kwa mzee huyo aliyefahamika kwa jina la Paul Kisiwa (72) mkazi wa kijiji cha Ng'ongo lilitokea machi 3 nyakati za jioni kwenye kijiji cha Kifinga Kata ya Mtowisa wilaya Sumbawanga. Taarifa kutoka eneo la tukio zilizothibitishwa na Diwani wa Kata ya Mtowisa, Edger Malinyi, zilieleza kuwa baada ya kuuawa kwa mzee huyo ambaye alikuwa Mwenyekiti wa CCM ngazi ya kata alizikwa kinyemela shambani kwake. Inaelezwa kuwa taarifa za kupotea mzee huyo zilianza kuzagaa ndipo ndugu wa marehemu pamoja na majirani  wakishirikiana na polisi walianza kuchunguza tukio hilo ambapo ilipofika machi 8 mwaka huu,watu hao walimbana mjukuu wa mzee huyo aitwaye John Kisiwa (22) ambaye alikiri kushiriki kupanga njama za kum...