Posts

CHAMA CHA ANC CHAAMUA ZUMA NI LAZIMA AONDOKE

Image
Chama tawala Afrika kusini African National Congress (ANC) kimemuomba rasmi rais Jacob Zuma ajiuzulu baada ya yeye kukataa kufanya hivyo mapema hii leo. Taarifa kuhusu uamuzi huo umefuata mfululizo wa mazungumzo ya maafisa wa juu wa chama hicho yalioendelea usiku kucha hadi kuamkia alfajiri ya leo. Haki miliki ya picha Muhula wa Zuma unamalizika mwaka ujao Iwapo Bw.Zuma(75) hatoteteleka atakabiliwana na kura ya kutokuwa na imani naye bungeni ambayo anatarajiwa kushindwa. Akiwa amehudumu madarakani tangu 2009, ameandamwa kwa tuhuma za rushwa. Haki miliki ya picha Imebainika kuwa mrithi wake Zuma atakuwa Cyril Ramaphosa kwasababu ndiye rais wa chama cha ANC. Chama cha ANC hakijathibitisha rasmi mipango yake lakini duru kutoka cham hicho zimetoa ufafanuzi katika vyombo vya habari nchini Afrika kusini na pia kwa shirika la habara la kimataifa la Reuters. Rais Zuma amekiuka shinikizo linaloongezeka la kumtaka ajiuzulu tangu Desemba wakati Cyril Ramaphosa alipoichukua nafa...

MWANASHERIA MKUU WA KENYA PROFESA GITHU MUIGAI ABWAGA MANYANGA

Image
Mwanasheria mkuu wa Kenya Profesa Githu Muigai amejiuzulu baada ya kuhudumu kwa miaka sita na nusu ambapo kufuatia uamuzi huo Rais Uhuru Kenyatta amemshukuru Profesa Githu kwa huduma zake na sasa jaji Paul Kihara Kariuki atachukua mahala pake. Kabla ya uteuzi wake kuwa mwanasheria mkuu profesa Muigai alikuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni ya mawakili ya Mohammed Muigai na amekuwa mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa katika kukabiliana na ubaguzi wa rangi. Haki miliki ya picha Mwanasheria mkuu wa Kenya Professa Githu Muigai Aidha alikuwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha sheria cha Columbia mjini New York ambapo Kutoka 1984 alikuwa mwanfunzi katika chuo cha kusomea uanasheria nchini Kenya . Wakati huo huo alikuwa mwanafunzi wa chuo kikuu cha Nairobi huku akiwa mshauri wa serikali katika maswala ya kisheria, Githu Muiga atakumbukwa kwa kuleta sheria za mageuzi katika timu ya uchaguzi nchini Kenya siku chache tu kabla ya uchaguzi kufanyika. Katika sheria hiyo kamishna yeyote yul...

WANAFUNZI WA SEKONDARI WASOMEA KATIKA VYUMBA VYA MAABALA

Image
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kasokola iliyopo Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,wanalazimika kusomea katika vyumba vya maabala vyenye kemikali za kisayansi zinazotumika kwa ajili ya masomo ya fikizikia,Kemia na baiolojia. Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wameiomba serikali na wadau kujenga vyumba vya madarasa ili kuwaepusha na mazingira hatarishi walimu na wanafunzi. Kwa upande wake Kaimu mkuu wa shule ya sekondari Kasokola Joel Mwandwanda amesema wanafunzi kusomea katika vyumba vya maabala kunatokana na uhaba wa vyumba vya madarasa katika shule hiyo ambapo hata walimu wamegeuza maabala hizo na baadhi ya vyumba vya madarasa kuwa ofisi.

ANC CHAADHIMISHA MIAKA 100 YA KUZALIWA KWA NELSON MANDELA

Image
Chama tawala cha Africa Kusini ANC kimeanza maadhimisho ya kumbukumbu za miaka mia moja tangu kuzaliwa kwa Raisi wa kwanza mweusi nchini humo shujaa Nelson mandela. Nelson Mandela Kiongozi wa sasa wa ANC ,Cyril Ramaphosa anatarajiwa kutoa hotuba huko medani mwa Freedom square mjini Cape Town, ambako marehemu Mandela alitoa hotuba yake ya kwanza alipoachilia huru kutoka gerezani miaka ishirini na nane iliyopita.

DR. SHEIN AAGIZA WIZARA YA ELIMU KULIPA MADENI YOTE YA WALIMU KABLA 2019

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein amesema sera ya elimu bure  kwa wanafunzi wa sekondari itaanza ifikapo  mwezi june  mwaka huu. Akizungumza  katika Mkutano Mkuu wa Sita wa chama cha walimu Zanzibar zatu amesema serikali imeamua  kuondoa ada  kwa wanafunzi  kwa lengo la kuendeleza sera ya rais wa awamu ya kwanza Shekh Abeid Amani Karume.

RAIS MAGUFULI AMPANDISHA CHEO NA KUMTEUA KAMISHNA WA POLISI ZANZIBAR

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli amempandisha cheo na kumteua Bw.Mohamed Hassan Haji kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar. Taarifa ambayo imetolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imefafanua kuwa Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo Bw.Mohamed Hassan Haji kutoka Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) na kuwa Kamishna wa Polisi (CP)na kisha kumteua kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar. Kamishna wa Polisi Mohamed Hassan Haji amepandishwa cheo na kuteuliwa kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar kuanzia leo Februari 10 ambapo kabla ya uteuzi huu Kamishna wa Polisi Mohamed Hassan Haji alikuwa Mhasibu Mkuu wa Polisi Zanzibar. Kamishna wa Polisi Mohamed Hassan Haji anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Kamishna wa Polisi Hamad Omar Makame ambaye amestaafu. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

TANZANIA YARIDHIA KUFUTA TOZO YA DOLA ZA KIMAREKANI

Image
Tanzania imeridhia kufuta tozo ya Dola za Kimarekani 40 inayotozwa kwa kila stika katika magari yanayosafirisha mizigo kwenda nje ya nchi. Hatua hii imefikiwa katika Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara,Viwanda,Fedha na Uwekezaji la Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao umeafnyika Jijini Arusha Akizungumza katika Mkutano huo,Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe.Charles Mwijage amesema Tanzania imefikia hatua hii ikiwa ni moja ya jitihada za kuendelea kuboresha mazingira ya biashara nchini na Jumuiya kwa ujumla. Tozo hii imekuwa ikitozwa kwa kipindi cha muda mrefu kwa malori yanoyosafirisha mizigo kwenda sehemu mbalimbali nje ya mipaka ya nchi. Mkutano huu uliofanyika Februari 7 mpaka 9 mwaka huu pamoja na mambo mengine ulilenga kujadili na kutatua vikwazo vya kibiashara visivyo vya kiushuru ambavyo vimekuwepo kwa muda mrefu katika Jumuiya. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED