MWANASHERIA MKUU WA KENYA PROFESA GITHU MUIGAI ABWAGA MANYANGA
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
Mwanasheria mkuu wa Kenya Profesa
Githu Muigai amejiuzulu baada ya kuhudumu kwa miaka sita na nusu ambapo
kufuatia uamuzi huo Rais Uhuru Kenyatta amemshukuru Profesa Githu kwa huduma
zake na sasa jaji Paul Kihara Kariuki atachukua mahala pake.
Kabla ya uteuzi wake kuwa mwanasheria
mkuu profesa Muigai alikuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni ya mawakili ya
Mohammed Muigai na amekuwa mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa katika kukabiliana
na ubaguzi wa rangi.
Haki miliki ya picha Mwanasheria mkuu wa Kenya Professa Githu Muigai
Aidha alikuwa mwanafunzi katika chuo
kikuu cha sheria cha Columbia mjini New York ambapo Kutoka 1984 alikuwa
mwanfunzi katika chuo cha kusomea uanasheria nchini Kenya .
Wakati huo huo alikuwa mwanafunzi wa
chuo kikuu cha Nairobi huku akiwa mshauri wa serikali katika maswala ya
kisheria, Githu Muiga atakumbukwa kwa kuleta sheria za mageuzi katika timu ya
uchaguzi nchini Kenya siku chache tu kabla ya uchaguzi kufanyika.
Katika sheria hiyo kamishna yeyote
yule katika tume ya uchaguzi alipewa nguvu za kumtangaza mshindi wa uchaguzi
iwapo mwenyekiti wa tume hiyo hayupo.
Sheria hiyo ilizua pingamizi kutoka
kwa upinzani pamoja na jamii ya kitaifa waliodai kuwa serikali haiwezi kufanya
mabadiliko ya sheria za uchaguzi wakati ambapo uchaguzi mkuu unakaribia.
Katika hatua nyingine Githu Muigai
atakumbukwa katika hatua ya
kuliharamisha kundi la upinzani la NRM hatua ambayo pia ilipingwa na viongozi
wa upinzani wakisema kuwa ni hatua mojawapo ya serikali ya kutaka kukandamiza
upinzani.
Siku chache kabla ya kiongozi wa
upinzani Raila Odinga aliyejiita kuwa 'rais wa wananchi' kula kiapo,Bwana Githu
alitishia kuwa mtu atakayejaribu kula kipao cha urais atajilaumu mwenyewe kwa
kuwa mashtaka yatakayomkabili ni ya uhaini ambao hukumu yake ni mtu kunyongwa.
Hatahivyo Raila alikula kiapo hicho
katika bustani ya Uhuru Park katika hafla iliohudhuriwa na maelfu ya wafuasi wa
upinzani na matokeo yake yalisababisha viongozi wa karibu walioshiriki katika
kumlisha bwana Raila Kiapo hicho kukamatwa na kushatkiwa huku wengine
wakifurushwa kutoka nchini.
Hatahivyo viongozi wengine wakuu wa
upinzani hawakuhudhuria hafla hiyo.
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga Jumanne aliapishwa kuwa 'rais wa wananchi' nchini humo baada ya kusema hatambui ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa marudio uliofanyika nchini humo Oktoba mwaka jana. Mgombea mwenza wake Kalonzo Musyoka wa chama cha Wiper hakujitokeza kwa sherehe hiyo ya kuapishwa, ingawa alikuwa miongoni mwa waliotarajiwa kuapishwa. Bw Odinga alisema Bw Musyoka, ataapishwa "baadaye". Waziri mkuu huyo wa zamani hayuko peke yake katika kujaribu kujitangaza marais, kukiwa bado kuna rais mwingine madarakani. Raila Odinga Akiapa Wengine ni akina nani? Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Etienne Tshisekedi, Nigeria Moshod Abiola, Uganda Kiza Besigye na Jean Ping wa Gabon ni miongoni mwa viongozi wa upinzani wa Afrika ambao wamejaribu kujitangaza kuwa marais, na sasa Raila Odinga amejiunga na orodha hii. Etienne Tshisekedi Etienne Tshisekedi Etienne Tshisekedi alikuwa kiongozi mkuu wa upinza...
Na.Issack Gerald Bathromeo-Tanganyika Kijiji cha Majalila kilichopo kata ya Tongwe Halmshauri Mpya ya Tanganyika Mkoani Katavi, kimetangazwa Rasmi kuwa Makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika.
Abdulrahman Kinana alizaliwa mwaka 1952 mkoani Arusha Arusha Kaskazini mwa Tanzania. Kinana ni mwanasiasa aliyeshika nyadhifa mbalimbali serikalini. Alihitimu shahada yake katika Chuo Kikuu cha Havard nchini Marekani akibobea kwenye masuala ya mikakati. Alikuwa Waziri wa ulinzi na Jeshi la kujenga taifa ,naibu Waziri wa mambo ya nje na uhusiano wa kimatafa na Waziri wa ulinzi. Kinana aliwahi kufanya kazi na Jeshi la wananchi la Tanzania kwa miaka 20 kabla ya kusaafu akiwa na cheo cha ukanali mwaka 1972. Abdulrahman Kinana pia aliwahi kuwa Spika wa Bunge la Afrika mashariki mwaka 2001 mpaka mwaka 2006. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED
Comments