Posts

WAUAWA KWA KUKATWA MAPANGA KWA MADAI YA USHIRIKINA

Image
Watu watatu wameuawa katika matukio tofauti likiwamo la wanawake wawili kuuawa kwa kukatwa mapanga kutokana na imani za kishirikina katika kitongoji cha  Kilombero Wilayani Nkasi mkoani Rukwa. Kamanda wa polisi Mkoani Rukwa George Kyando aliwataja waliouawa kuwa ni Salome Kisinza(50) na Rahel Pawa(22) walikatwa mapanga sehemu mbalimbali za miili yao na watu wasiojulikana. Kyando alisema waliofanya mauaji hayo waliwavizia wakiwa wamelala ndani ya nyumba yao ambapo walivunja mlango na kuingia ndani na kuanza kuwakata mapanga. Alisema walimuua Salome na kumjeruhi Rahel baadaye walitoweka huku wakimwacha katika hali mbaya na alifariki dunia akiwa njiani akipelekwa hospitali. Kamanda Kyando alisema chanzo cha mauaji hayo inasadikiwa ni tuhuma za imani za ushirikina kwa kuwa Salome alikuwa akituhumiwa kumroga mume wake Jilala Mponeja ambaye amekuwa akiumwa kwa muda mrefu na anatibiwa kwa mganga wa jadi wilayani Kalambo mkoani humo. Katika tukio jingine lililotokea s...

MKOA WA KATAVI KUUNGANISHWA NA GRID YA TAIFA

Image
WAZIRI wa Nishati Dr.Merdard Kareman   amesema m iaka miwili ijayo shirika la umeme Tanesco mkoa ni Katavi litakuwa limeunganisha Mkoa wa Katavi katika gridi ya taifa. Waziri Kareman  ametoa kauli hiyo wakati akikagua mradi wa mashine za kuzalisha umeme katika mji wa Inyonga wilaya ni. Amesema mpaka kufikia mwaka 2019 maeneo mengi hasa vijijini yatakuwa yameunganishwa na umeme ili kuongeza kasi ya uchumi wa viwanda mkoani Katavi. Kwa sasa Mkoa wa Katavi unatumia jenereta kuzalisha umeme unaotumika ktika wilaya za Mpanda,Mlele na Katavi ambapo wakazi wengi wamekuwa wakilalamikia tatizo la umeme jenereta linapokuwa na tatizo. Waziri Kareman  ambaye alifanya ziara Mkoani Katavi akitokea Mkoani Kigoma aliendelea na ziara Mkoani Rukwa. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

RAIS MAGUFULI ATOA AGIZO ZITO KWA KAMISHINA WA UHAMIAJI NCHINI

Image
Rais John Magufuli ameitaka Idara ya Uhamiaji kuhakikisha inapambana na wahamiaji haramu pasipo kumwogopa mtu. Amemwagiza Kamishna wa Uhamiaji,Dk Anna Makakala kuwachukulia hatua kali watumishi wake watakaoshindwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo. Rais Dkt.John Pombe Magufuli Dk.Magufuli akizungumza leo akizindua hati ya kusafiria ya kielektroniki jijini Dar es Salaam,amesema utambuzi wa wananchi wanaoishi bila vibali na wenye vibali vilivyoisha ni muhimu. Amesema uhamiaji ina jukumu kubwa katika kutekeleza hayo. Amesema awali Uhamiaji iligubikwa na matatizo yakiwamo ya utoaji hovyo wa vibali vya uraia, hata kwa watu ambao walikuwa hawana sifa. Dk Magufuli amesema hiyo ndiyo sababu iliyofanya akamteua Dk Makakala kuwa Kamishna. "Wanawake ni waaminifu sana na ameanza kutatua matatizo haya." Baadhi ya viongozi waliohudhuria uzinduzi huo ni Rais wa Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein,Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa. Wengine ni marais...

WIZARA YATOA TAMKO KWA WALIOPOTEZA VYETI VYAO VYA ELIMU

Image
Wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia imewataka watanzania wote nchini waliopoteza vyeti vyao vya elimu watoe taarifa mapema katika sehemu husika na wasisubiri mpaka pale wanapokuwa na uhitaji navyo ndio waanze kuhangaika. Mhe.William Ole Nasha Hayo yameelezwa leo Bungeni na Naibu Waziri Wizara ya hiyo Mhe.William Ole Nasha kwa niaba ya Waziri ya Waziri Sayansi,Teknolojia wakati alipokuwa anajibu swali lililoulizwa na Mbunge wa Mafinga Mjini Cosato David Chumi. Chumi alitaka kufahamu serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Elimu ina mpango gani wa kuwasaidia watanzania waliopoteza vyeti vyao vya elimu na kuvipata vingine. Kwa upande mwingine,Mhe.William Ole Nasha amesema muombaji wa cheti mbadala au uthibitisho wa matokeo hupatiwa huduma baada ya kumaliza utaratibu wote uliyowekwa na Wizara hiyo. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

SERIKALI YAKIRI KUDAIWA NA VIWANDA

Image
Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Mhe.Charles Mwijage amekiri ni serikali ya Tanzania kudaiwa na viwanda vya ndani. Mhe.Charles Mwijage  Amesema wanaosababisha deni lisilipwe ni watanzania wasiolipa kodi. Waziri Mwijage amebainisha hayo leo katika mkutano wa Bunge wa 10 kikao cha Pili kinachoendelea kufanyika mjini Dodoma. Waziri Mwijage alikuwa akijibu swali la nyongeza katika wizara yake ambapo aliulizwa kuwa serikali ina mkakati gani madhubuti wa kulipa madeni hayo ili kunusuru anguko la viwanda ambavyo vimeanzishwa kwa nia njema. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

MADIWANI WATATU CHADEMA WASIMAMISHWA

Image
Madiwani watatu wa CHADEMA halmashauri ya Mji wa Njombe wametolewa nje ya kikao cha baraza la madiwani na kusimamishwa kuhudhuria vikao 3 kutokana na kujadili mkataba wa halmashauri na kampuni iliyowekwa kukusanya ushuru ambayo inawanyanyasa wananchi. Madiwani hao ni pamoja na George Sanga diwani Kata Ramadhani,Sigrada Mligo,diwani viti maalum,Legnard Danda diwani kata Ihungilo. Madiwani hao walitolewa kwenye mkutano na kusimamishwa kuhudhuria vikao vitatu baada ya kuhoji mkataba wa halmashauri na kampuni ya Ihagara inayo kusanya ushuru mjini Njombe ambayo inadaiwa kuwanyanyasa wananchi.  Awali Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji wa Njombe, Edwin Mwanzinga alipiga marufuku kujadili suala hilo kwa madai kuwa baraza halina mkataba huo na hakuna palipo andikwa jina la kampuni hiyo. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

VIONGOZI WENGINE WALIOWAHI KUAPISHWA NA KUJITANGAZA KUWA MARAIS KAMA ODINGA BARANI AFRIKA

Image
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga Jumanne aliapishwa kuwa 'rais wa wananchi' nchini humo baada ya kusema hatambui ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa marudio uliofanyika nchini humo Oktoba mwaka jana. Mgombea mwenza wake Kalonzo Musyoka wa chama cha Wiper hakujitokeza kwa sherehe hiyo ya kuapishwa, ingawa alikuwa miongoni mwa waliotarajiwa kuapishwa. Bw Odinga alisema Bw Musyoka, ataapishwa "baadaye". Waziri mkuu huyo wa zamani hayuko peke yake katika kujaribu kujitangaza marais, kukiwa bado kuna rais mwingine madarakani. Raila Odinga Akiapa Wengine ni akina nani? Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Etienne Tshisekedi, Nigeria Moshod Abiola, Uganda Kiza Besigye na Jean Ping wa Gabon ni miongoni mwa viongozi wa upinzani wa Afrika ambao wamejaribu kujitangaza kuwa marais, na sasa Raila Odinga amejiunga na orodha hii. Etienne Tshisekedi Etienne Tshisekedi Etienne Tshisekedi alikuwa kiongozi mkuu wa upinza...