Posts

STENDI MPYA YA MABASI MPANDA KUANZA KUTUMIKA MWANZONI MWA 2018

Image
Na.Issack Gerald Mstahiki Meya wa M anispaa ya Mpanda mkoani katavi Willium Mbogo amesema stendi kuu ya mabasi ya kisasa inatarajiwa kuanza kufanya kazi mwanzoni wa mwaka 2018. Mh.Mbogo amesema hatua iliyobaki ni ujenzi wa vibanda na kukamilisha huduma ya maji na umeme. Aidha amesema stendi hiyo itakuwa na uwezo wa kuingiza mabasi 60 kwa wakati mmoja   ambapo ametoa wito kwa wamiliki wote wa mabasi kununua mabasi yanayoenda na hadhi ya stendi. Mkoa wa Katavi umefikisha miaka mitano toka kuanzishwa kwake huku ukipiga hatua kubwa ya kimaendeleo ukilinganisha na mikoa mingine michanga. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

ROBO YA MWAKA WA FEDHA 2017/2018 HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA IMETUMIA SHILINGI MIL.50 KWA VIKUNDI VYA UJASILIAMALI

Image
Na.Issack Gerald Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi,imefanikiwa kutoa mkopo shilingi milioni hamsini kwa vikundi vya wanawake na vijana katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2017/2018. Hayo yamebainishwa na Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Bi.Halima Kitumba wakati akizungumzia  kuhusu namna Halmshauri inavyotekeleza agizo la serikali kutumia asilimia 10 ya mapato ya ndani kuwawezesha wanawake na vijana. Katika mgao wa fedha hizo jumla ya vikundi 8 vya wanawake ambavyo vimepata shilingi milioni 29,700,000 huku vikundi 6 vya vijana vikipata miluioni 20,300,000. Aidha amesema katika robo ya pili inayoanzia mwezi Oktoba mwaka huu,wanatarajia kutumia shilingi milioni 50 kwa vikundi 19 ambapo mpaka sasa wametoa zaidi ya shilingi milioni 11,786,000/= zilizoelekezwa katika viwanda vidogo vidogo SIDO kwa ajili ya kununua vifaa vya uchakataji na kutoa mafunzo mbalimbali ya ujasiliamali kwa wanawake na vijana waliopo Iko...

MKOANI KATAVI DIWANI JELA MIAKA 3 KWA KUOMBA NA KUPOKEA RUSHWA

Image
Na. Issack Gerald Mahakama ya wilaya ya Mlele imemkumu kwenda jela diwani wa kata ya Katumba Senator  Jeriti Baraka kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa. Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama hiyo Timothy Swai, mwendesha mashtaka wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoa wa katavi Bahati Haule amedai mtuhumiwa alitenda kosa hilo 12.05.2016 kwa kuomba rushwa ya shilingi 500,000/=ili asimuhamishe mfugaji mmoja kwenye eneo lililozuiliwa na mahakama kuendesha shughuli za ufugaji. Taarifa iliyotolewa na  taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoani katavi imesema mtuhumiwa amehukumiwa kwa makosa mawili tofauti ambapo kosa la kwanza ni kuomba rushwa na kosa la pili ni kupokea rushwa. Taarifa hiyo inaeleza kuwa kosa la kuomba rushwa mtuhumiwa amehukumiwa kutoa faini ya shilingi 500,000/= au kifungo cha miaka mitatu na kosa la kupokea rushwa mtuhumiwa amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela bila faini. Katika taaifa ya Takukuru inaeleza kuwa b...

WAKAZI MKOANI KATAVI WAMESHAULIWA KUJIUNGA NA ASASI MBALIMBALI

Wananchi mkoani Katavi wameshauriwa kujiunga na asasi mbalimbali za kimaendeleo ili kujikwamua kiuchumi. Wito huo umetolewa na Emiliana Stanslaus, mkufunzi wa asasi isiyo ya kiserikali ya Tanzania Girl Guides Association wakati wa uzinduzi wa kampeni maalum ya You Report kwa ajili ya kutoa taarifa mbalimbali kwa njia ya ujumbe mfupi. Kwa upande wake mgeni rasmi katika hafla hiyo Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoani Katavi  Bi Anna Shumbi amewataka wananchi kutumia fursa hiyo ili waweze kuandaa maisha yao ya baadae kulingana na dhima ya chama ya kuwainua kiuchumi Tanzania Girl Guides Association imelenga kuwaendeleza wasichana na wanawake  katika masuala  mbalimbali ya kijamii na kiuchumi Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

RC KATAVI AWATAKA WANANCHI KUCHANGAMKIA KILIMO CHA PAMBA NA KOROSHO

Image
Mkuu wa mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga amewataka wananchi kuchangamkia kulima kilimo cha korosho na pamba. Korosho  Ametoa kauli hiyo wakati wa kukabidhi hundi kwa vikundi vya akina mama na vijana wasiriamali  ambapo jumla ya milioni 37 zimetolewa kwa vikundi 12. Pamba Ameongeza kuwa  upatikanaji wa mbegu za mazao hayo ni wa uhakika na tayari mkoa wa Katavi umepokea tani 51 za mbegu ya pamba kutoka bodi ya pamba Tanzania Huu ni mkakati wa Mkoa wa katavi kuondoa utegemezi wa zao la tumbaku ambalo limekumbwa  na changamoto ya kukosekana wanunuzi . Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

RAIS MAGUFULI AWAONYA MASHA NA MSANDO,SOFIA SIMBA NAYE ASAMEHEWA WOTE WARUHUSIWA KUGOMBEA NYADHIFA MBALIMBALI NDANI YA CHAMA

Image
Na.Issack Gerald Mwenyekiti wa CCM Rais John Magufuli Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Rais John Pombe Magufuli amewaonya wanachama wapya ambao wamehamia ndani ya chama hicho leo kwenye mkutano mkuu wa NEC ambao umefanyika Ikulu jijini Dar es salaam. Kutoka Kulia ni Bw.Laurenance Masha na anayefuata ni Alberto Msando Wanachama hao ambao wamehamia na kutangazwa leo ni Mwanasheria Alberto Msando aliyekuwa mwanachama wa ACT-Wazalendo,Mbunge wa zamani wa Nyamagana Laurent Masha aliyekuwa mwanachama wa Chadema pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la vijana Chadema taifa Patrobas Katambi. Wengine ni Profesa Kitila Mkumbo ambaye naye alikuwa mwanachama wa ACT-Wazalendo pamoja na Sophia Simba ambaye ameomba kurejeshewa uanachama baada ya kufukuzwa kwa muda. Rais Magufuli amemaliza kwa kuwapa ruhusa ya kugombea nyadhifa mbalimbali ndani ya chama na kwenye maeneo yao. Kwa upande wake aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA Lawrence Masha ambaye ametangaza kukihama chama hiko hivi ka...

HABARI ZA HIVI PUNDE KUTOKA IKULU

Image
Serikali imekanusha taarifa zinazoenezwa kupitia mitandao ya kijamii kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt.Laurian Ndumbaro. Kwa mjibu wa taarifa ambayo imetolewa na mkurugenzi wa mawasiliano ikulu ya rais Bw.Gerson Msigwa amesema taaifa hizo  sio za kweli  na  zipuuzwe . Taarifa hiyo inaeataka wananchi kuendelea kupokea taarifa rasmi kutoka kwenye mamlaka na vyombo rasmi vya Serikali. Wakati huo huo watumiaji wa mitandao ya kijamii wamekumbushwa kumbushwa kuwa kueneza taarifa za uongo ni makosa kisheria. Hata hivyo,Serikali imesema itawafuatilia wote waliozusha taarifa hizi na kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED