Posts

BARAZA LA MADIWANI HALMSHAURI YA WILAYA YA MPANDA KUFANYA KIKAO CHAKE KESHO,SHILINGI MIL.120 ZILIZOTUMIKA KINYUME NA MALENGO,BARAZA LA MADIWANI KUTOA TAMKO

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Mpanda Katavi BARAZA la madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Wilayani Tanganyika Mkoani Katavi,kesho linatarajia kufanya kikao chake cha robo ya mwaka kwa mwaka 2016 ambapo masuala mbalimbali yatajadiliwa ikiwemo kutoa   tamko la kubadilishwa matumizi ya Shilingi milioni 120 zilizokuwa zitumike kununulia gari la Mkurugenzi mtendaji wa Halmshauri hiyo ambapo zilitumika kwa ajili ya Masuala ya mitihani. Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Mpanda Mh.Hamad Hassan Mapengo(PICHA NA.Issack Gerald)                                                 

SHIRIKA LA UNHCR KESHO KUKABIDHI GARI KWA JESHI LA POLISI MKOANI KATAVI KUSAIDIA KUIMARISHA ULINZI NA USALAMA

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Mpanda Katavi SHIRIKA la wakimbizi duniani UHNCR Mkoani Katavi,kesho linatarajia kukabidhi gari kwa jeshi la Polisi Mkoani Katavi ili kurahisisha shughuli za ulinzi na usalama za jeshi hilo.                                           

WALEMAVU WASIOONA 127 WAKIWEMO WANAFUNZI 58 MKOANI KATAVI BADO WANA MATATIZO MAKUBWA YA KUKOSA HUDUMA STAHIKI KATIKA ELIMU NA AFYA

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Katavi CHAMA cha Wasioona Tanzania TLB Mkoani Katavi,kimesema Walemavu zaidi ya 127 wasioona waliopo Mkoani Katavi,bado wanakabiliwa na hatari ya kukosa huduma muhimu mbalimbali kama elimu,afya na mengineyo muhimu kutokana na jamii kuendelea kuwa na mtazamo kuwa,walemavu hawana mchango wa kuleta maendeleo. Naibu Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Tulia Akson akihutubia siku ya fimbo nyeupe Mkoani Mbeya akiwa ndiye Mgeni rasmi(PICHA NA.Issack Gerald) Bw.Emmanuel Simon katibu wa TLB taifa akiwasilisha taarifa wakati wa maadhimisho ya siku ya wasioona maarufu siku ya fimbo nyeupe Mkoani Mbeya(PICHA NA.Issack Gerald)                              

MKUU WA WILAYA YA TANGANYIKA AVUNJA BODI YA CHAMA WAKULIMA WA TUMBAKU MISHAMO TAMCOS

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Tanganyika MKUU wa wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi Saleh Mbwana Mhando,ameivunja bodi ya chama cha wakulima cha tumbaku MISHAMO TAMCOS na kuamru viongozi wote wa bodi hiyo wakamatwe haraka.                                              Wakulima wa Chama cha Ushirika Mishamo Tamcos katika picha wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika pichani hayupo Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Saleh Mbwana Mhando akizungumza na wakulima wa chama cha Ushirika MISHAMO TAMCOS(Picha na Issack Gerald) Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika cha MISHAMO TAMCOS Bw. Bw.Pridas Amakredo(picha na Issack Gerald)

MKUU WA MKOA WA KATAVI APOKEA SHILINGI 500,000/= KUTOKA MUKABUBINGA KWA AJILI WAATHIRIKA TETEMEKO LA ARDHI KAGERA,FEDHA ILIYOCHANGWA YAFIKIA MIL. 13,344,600 KUWASILISHWA KAGERA JUMATATU.

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo - Katavi MKUU wa Mkoa wa Katavi Meja Jeneral mstaafu Raphael Muhuga amepokea Shilingi laki tano kutoka kwa MUKABUBINGA ambao ni Umoja wa wanakagera waishio Wilayani Mpanda ambapo fedha hiyo ni kwa ajili ya kuwachangia waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi na Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda(PICHA NA.Issack Gerald) Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jeneral Mstaafu Raphael Mugoya Muhuga(PICHA NA.Issack Gerald)                    

TCCIA KATAVI : SERIKALI ITAFUTE MFUMO WA KUDUMU KUSIMAMIA SEKTA YA KILIMO,MENEJA MPANDA KATI NAYE ASEMA UZALISHAJI WA TUMBAKU UMEPUNGUA KUTOKA KILO 3.5 - 1.4 MILIONI

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Mpanda Katavi CHAMA cha watu wenye kilimo,viwanda na Biashara TCCIA Mkoani Katavi,kimeishauri serikali kutafuta mfumo wa kudumu utakaosimamia sekta ya kilimo ikiwemo kusimamia mfumo wa usambazaji wa pembejeo za kilimo hapa nchini ili wakulima walime kilimo chenye tija kwao kutokana na matumizi sahihi ya pembejeo hizo ikiwa zitaletwa kwa wakati.                                             

ASILIMIA 45 YA WATOTO CHINI YA MIAKA 18 TANZANIA HUPATA UJAUZITO NA KUPOTEZA MAISHA WAKATI WA KUJIFUNGUA

Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama -Nkasi Rukwa Asilimia 45 ya watoto wa kike waliochini ya  umri wa miaka 18 hupata ujauzito na kupoteza maisha kila mwaka  wakati wa kujifungua kwa mjibu wa  utafiti uliofanywa  na Shirika lisilokuwa la kiseriklai la Plan International Tanzania.