Posts

NYUMBA ILIYOTEKETEA KWA MOTO JUZI ,CHUMBA CHA MPANGAJI HASARA NI ZAIDI YA MILIONI MOJA NA LAKI TANO(1,500,000).

Na.Issack Gerald Bathromeo-Mpanda Imebainika kuwa janga la moto lililotokea juzi katika Mtaa wa Mpadeco Kata ya Mkananyagio Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,umesababisha Bi.Grace Emmanuel Mkazi wa mtaa wa Mpadeco kata ya Makanyagio kupata hasara ya Zaidi ya Shilingi Miloni moja na laki tano (1,500 ,000). B.Grace amesema Moto huo uliozuka mchana uliunguza Vitanda 2 vyenye thamani ya laki tano na elfu sitini(560,000),Magodoro mawili 5 kwa 6 yenye thamani ya Shilingi laki tatu(300,000),Maguni ya Mpunga 4 thamani yake zaidi ya Shilingi laki 2(200,000),Upotevu wa fedha taslimu Shilingi laki nne na nusu za mkopo zilizopotea wakati wa uokozi na nguo ambazo tahamani yake haijafahamika. Akizungumza akiwa nyumbani kwake muda mfupi baada ya kutoka hospitali ya Wilaya ya Mpanda,alikolazwa baada ya kuzimia kutokana mshtuko alioupata baada ya kupata hasara hiyo,amesema kuwa hata hivyo hajatambua kiasi alichotumia kwa ajili ya matibabu. Hata hivyo amekwishafungua jarada Polisi ili ili kufany...

NYUMBA YATEKETEA KWA MOTO MPANDA

Na.Issack Gerald Bathromeo-Mpanda Moto umeunguza nyumba ya Familia moja na kusababisha hasara ya mali ambayo thamani yake haijajulikana katika mtaa wa Migazini kata ya Makanyagio   Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi.

MKUU WA WILAYA TANGANYIKA:ENEO LA LUHAFE SASA KUJENGWA MJI WA MAKAZI NA BIASHARA.

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Tanganyika MKUU wa Wilaya ya Tanganyika Bw.Salehe Mbwana Mhando,ametangaza wakazi wa eneo la Luhafe lililopo kata ya Majalila,kulitumia eneo hilo kwa makazi na shughuli za kibiashara baada ya mgogoro wa uhalali wa eneo hilo wa muda mrefu. Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Bw.Saleh Mbwana Mhando akihutubia wakazi wa kitongoji cha Luhafe(PICHA NA.Issack Gerald)Septemba 16,2016                                                                           

VIJIJI ZAIDI YA 14 VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO KUPATA UMEME WA REA AWAMU YA III MWAKA 2016

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Mpanda,Katavi Meneja wa TANESCO mkoa wa Katavi Mhandisi Julius Sabu amesema katika awamu ya tatu ya umeme wa REA wanampango wa kusambaza umeme katika vijiji ambavyo havikupitiwa na mpango huo katika awamu zilizopita.                                    

WAKAZI WILAYANI TANGANYIKA WAAGIZWA KUONGEZA KASI YA KUJENGA SEKONDARI KILA KATA

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Tanganyika WAKAZI wilayani Tanganyika Mkoani Katavi kwa Kushirikiana na uongozi wa vijiji na kata   katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika,wameagizwa kuweka mikakati ya ujenzi wa shule za Sekondari kila kata ,ili kila mwanafunzi asome bila kuhangaika na badala yake apate elimu bora.                                       Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Saleh Mbwana Mhando akishiriki ujenzi Shule ya sekondari ya Bulamata  kata ya Bulamata(PICHA NA Issack Gerald)Septemba 16,2016                                          Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika akizungumza na wananchi eneo la kijiji cha Busongola kunakojengwa Shule ya Sekondari Bulamata(P...

MKUU WA WILAYA YA TANGANYIKA AAGIZA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 200 ZA WAKULIMA WA ZAO LA TUMBAKU CHAMA CHA USHIRIKA TAMCOS KULIPWA NDANI YA SIKU 15.

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Tanganyika MKUU wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi Bw.Saleh Mbwana Mhando,ameuagiza uongozi wa bodi ya Chama cha Msingi cha Ushirika TAMCOS na Afisa Ushirika Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Bw.Luxford Mbunda,kuhakikisha wanalipa   zaidi ya Shilingi milioni 200 wanazodai wakulima wa zao la tumbaku wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kwa misimu 3 ya kilimo kuanzia mwaka 2011-2015 kabla ya Septemba 30 mwaka huu. Baadhi ya Wakulima wa Zao la Tumbaku wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika(hayupo pichani) katika Ofisi za TAMCOS Mishamo(PICHA NA.Issack Gerald) Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Saleh Mbwana Mhando Aliyesimama akihutubia wakulima wa tumbaku wa chama cha Msingi cha Ushirika TAMCOS Mishamo(PICHA NA.Issack Gerald)                                       Wakulima wa chama cha Msingi cha Ushirika TAMCOS Mishamo wakimsikiliza Mkuu ...

KIFO CHA MTU KUJINYONGA KATAVI,NDUGU,MASHUHUDA WASIKITIKA

Image
Na.Issack Gerald Bathromeo-Katavi MTU mmoja anaekadiliwa kuwa na umri wa miaka 30 Innocent Milambo mkazi wa mtaa wa kigoma kata ya Makanyagio wilayani Mpanda   mkoani Katavi,amekutwa amekufa kwa kujinyonga   usiku wa kuamkia leo kwa kile kinachodaiwa kuwa ni imani za kishirikina. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Katavi ACP Damasi Nyanda(PICHA NA.Issack Gerald)