MKUU WA WILAYA YA TANGANYIKA AAGIZA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 200 ZA WAKULIMA WA ZAO LA TUMBAKU CHAMA CHA USHIRIKA TAMCOS KULIPWA NDANI YA SIKU 15.


Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Tanganyika
MKUU wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi Bw.Saleh Mbwana Mhando,ameuagiza uongozi wa bodi ya Chama cha Msingi cha Ushirika TAMCOS na Afisa Ushirika Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Bw.Luxford Mbunda,kuhakikisha wanalipa  zaidi ya Shilingi milioni 200 wanazodai wakulima wa zao la tumbaku wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kwa misimu 3 ya kilimo kuanzia mwaka 2011-2015 kabla ya Septemba 30 mwaka huu.
Baadhi ya Wakulima wa Zao la Tumbaku wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika(hayupo pichani) katika Ofisi za TAMCOS Mishamo(PICHA NA.Issack Gerald)
Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Saleh Mbwana Mhando Aliyesimama akihutubia wakulima wa tumbaku wa chama cha Msingi cha Ushirika TAMCOS Mishamo(PICHA NA.Issack Gerald)
                                     
Wakulima wa chama cha Msingi cha Ushirika TAMCOS Mishamo wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika(hayupo pichani) katika mkutano wa hadhara uliofanyika Septemba 15,2016 katika ofisi cha Chma hicho(PICHA NA.Issack Gerald)

Bw.Mhando ametoa agizo hilo leo katika mkutano wa hadhara ambao ameufanya baina yake na wakulima  wa zao la tumbaku wa Chama cha Msingi cha Ushirika TAMCOS kilichopo kata ya Mishamo Halmshauri ya Wilaya ya Tanganyika.
Aidha,aMkuu wa Wilaya mesema,serikali ya Wilaya ya Tanganyika haitamvumilia mtendaji au mtumishi yeyote wa Halmshauri hiyo,ambaye atasababisha wananchi kunyanyasika katika haki zao,wakati nguvu kubwa imetumika katika uzalishaji.
Kwa upande wa Meneja wa TAMCOS,Bw.Valaniho Gataro,Mwenyekiti wa Chama cha Msingi cha Ushirika TAMCOS Bw.Pridas Amakredo na Afisa Ushirika Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ambaye pia ndiye anayeshughulikia vyama vya ushirika vilivyopo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Bw.Luxford Mbunda,wakijibu hoja za wakulima wa zao hilo katika Mkutano huo,hoja zao zilikataliwa na wakulima wa hilo kwa madai kuwa majibu ya madai yao yanajibiwa isivyo.
Wakulima mbali na kudai kiasi cha zaidi ya Shilingi Milioni 200, zilizotokana na mauzo ya zao la tumbaku,pia wamedai bodi ya chama cha TAMCOS ivunjwe ili kuchagua viongozi wengine,kwa kuwa uongozi uliopo madarakani upo kwa ajili ya kuwaibia fedha wanazotakiwa kupewa wakulima.
Aidha wakulima hao,wamewatuhumu viongozi wa TAMCOS kuwafutia usajili baadhi ya wakulima wanaoonekana kuhoji maslahi yao,ambapo baada ya kufutwa imegundulika kuwa wakulima wanazuiwa kushiriki kilimo cha zao hilo ikiwemo kunyimwa pembejeo licha ya kuwa na haki ya kupatiwa pembejeo hizo.
Wakati huo huo wakulima wamelalamikia upandaji miti hewa uliofanywa na mkandarasi aliyepewa tenda ya kupanda miti, kutokana na malipo ya fedha za wakulima wa Chama Cha TAMCOS licha ya kuwa fedha alikwishalipwa.
Habari hii pia ipate kupitia P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM
Kwa maoni au ushauri au ukiwa na habari yoyote tuma kupitia p5tanzania@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA