Posts

MATUKIO YA WIKI MKOANI KATAVI NA TANZANIA KWA UJUMLA DESEMBA 21-26,2015 NA P5 TANZANIA YA ISSACK GERALD BATHROMEO

 NA.ISSACK GERALD BATHROMEO MAUAJI KATAVI Posted By: Issack Gerald | At: Monday, December 21, 2015 Na.Issack Gerald- Katavi Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la   KAZIMIRI MASUMBUKO(49) MKAZI NA MKULIMA WA MISANGA aliuawa kwa kuchomwa kitu chenye ncha kali sehemu za mgongoni, mkononi, mkono wa kushoto na kidevuni na watu wasiofahamika Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo,Kmanda wa Polisi Mkoani Katavi Dhahiri Kidavashari,amesema tukio hilo limetokea jana Jumapili tarehe 20.12.2015 majira ya saa katika kitongoji cha Misanga Kata na Tarafa ya Mwese Wilayani Mpanda Mkoani Katavi. Kamanda Kidavashari amesema kuwa, siku ya tukio hilo,watuhumiwa wasiofahamika kwa sura wala idadi yao walifika nyumbani kwa marehemu wakakuvunja mlango na kuingia moja kwa moja hadi chumbani kwa marehemu na kumpeleka sebureni kwake kisha kutekeleza mauaji hayo na kutokomea kusikojulikana . Mpaka sasa chanzo cha tukio hilo bado hakijafahamika. Hata hivyo Upelelezi wa shauri hi...

WATATU KATAVI WASHIKILIWA NA POLISI KWA KUKUTWA NA NYARA ZA SERIKALI

Na.Issack Gerald-Mpanda Jeshi la polisi Mkoani Katavi linawashikilia watu watatu kutokana na kukamatwa na nyara za serikali ambazo wamezipata kinyume na sheria.

KAMANDA WA POLISI MWANZA ATOA TAARIFA YA ASKARI KUMUUA KWA RISASI ASKARI MWENZAKE

NA.Mwandisi wetu-MWANZA Askari mmoja  wa jeshi la Polisi mkoani Mwanza  jana amefyatua risasi na kumuua asikari mwenzake kisha nayeye kujipiga risasi na kufariki dunia katika lindo la benki ya posita jijini mwanza huku chanzo cha tukio hilo kikiwa hakija julikana.

AKIMBIA MKONO WA POLISI KUKWEPA KUKAMATWA KWA KOSA LA KUMILIKI SILAHA KINYUME NA SHERIA

Na.Issack Gerald-Mpanda Jeshi la polisi Mkoani Katavi linamtafuta mtu mmoja aliyekimbia akikwepa kukamatwa na polisi kutokana na kumiliki silaha aina ya gobore  kinyume na sheria.

AFARIKI DUNIA BAADA YA KUFUKIWA NA KIFUSI AKICHIMBA DHAHABU NSIMBO KATAVI

Na.Issack Gerald-Mpanda Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina Mateo Robert(33) mchimbaji mdogo mkazi wa Mbeya-Songwe,amefariki dunia baada ya kuangukiwa na lundo la udongo akiwa kwenye shimo (LONG BASE) wakati akichimba madini ya dhahabu.

BODABODA MPANDA WAZUNGUMZIA MIUNDOMBINU MIBOVU YA BARABARA INAVYOATHIRI UCHUMI WAO

Na.Issack Gerald-MPANDA Miundombinu mibovu ya barabara hususani kipindi hiki cha masika imeathiri uchumi wa waendesha pikipiki katika Manispaa ya Mpanda Mkoani Matavi.

WAKUU WA MIKOA,WILAYA NA WAKURUGENZI HALMASHAURI NCHINI WATAKIWA KUDHIBITI MIGOGORO YA ARDHI

Image
Na. OFISI YA WAZIRI MKUU,   WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha kuwa wanaongeza udhibiti na usimamizi wa migogoro ya  ardhi kwenye maeneo yao husika.                                                                  Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majliwa akisalimia na waakazi Jimboni Kwake Ruangwa