Posts

KAKESE,MWAMKURU WATAHADHARISHWA KIPINDUPINDU WAASWA KUDUMISHA USAFI

Na.Issack Gerald-MPANDA. WANANCHI wa Kata ya Kakese na Mwamkulu katika Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wametakiwa kuzingatia usafi ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu.

UONGOZI SOKO KUU MPANDA WAKANUSHA KUTOZA USHURU MARA MBILI,KUTO TOA RISITI NA UNYANYASAJI

Na.Issack Gerald-MPANDA Uongozi wa soko kuu lililopo Wilayani Mpanda Mkoani Katavi umekanusha madai yaliyotolewa na wafanyabiashara wa soko hilo kuhusu kutozwa ushuru mara mbili na wasimamizi wa soko hilo.

UZINDUZI MATUMIZI YA MIZANI,TAASISI ZA SERIKALI NA BINAFSI ZAASWA KUHAMASISHA MATUMIZI YA VIPIMO HALALI KATIKA BIASHARA

Image
Mmoja wa wakazi wa Mpanda akionesha kauli mbiu ya hapa kazi tu siku ya uzinduzi wa wakala wa vipimo katika viwanja vya soko la Buzogwe Manispaa ya Mpanda (PICHA na Issack Gerald) Mkuu wa Wilaya ya Mlele Kanal Issa Seleman Njiku akimkabidhi mzani mfanyabiashara mdogo kama ishara ya kuzindua matumizi ya mizani Mkoani katavi yaliyofanyika leo katika viwanja vya soko la Buzogwe (Picha Issack Gerald) Kikao cha wakala wa vipimo na waandishi wa habari,katikakati ni Irene John Kaimu meneja wa Sehemu ya elimu habari na mawasiliano wa wakala wa vipimo kutoka makao makuu Dar Es salaam,Mwenye T-shirt Nyekundu ni Moses Ezekiel Ntungi,Mratibu wa Programu ya Ukopeshaji mizaniaMkoani Katavi  na aliyevaa koti ni Abnery Amos Nzaga Meneja wa Mkoa wakala wa vipimo Rukwa na Katavi (PICHA NA Issack Gerald) Baadhi ya wafanyabiashara katika uzinduzi wa matumizi ya vipimo(mizani) katika biashara (PICHA na Issack Gerald) Na.Issack Gerald-MPANDA Taasisi binafsi na serikali...

MKURUGENZI APEWA AGIZO KUSIKILIZA CHANGAMOTO ZA WAFANYABIASHARA SOKO LA BUZOGWE

Na.Issack Gerald-MPANDA Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda amepewa siku moja kuhakikisha anafika soko la Buzogwe kuchunguza changamoto za ukosefu wa umeme,ulinzi wa biashara na maji zinazowakabili wafanyabiashara waliopo katika soko hilo.

WANNE MBARONI KATAVI AKIWEMO MWENYE NYARA ZA SERIKALI ZENYE THAMANI YA SHILINGI MIL.60

Na.Issack Gerald-MLELE Jeshi la Polisi Wilayani Mlele Mkoani Katavi kwa kushirikiana na askari wa Hifadhi ya Taifa ya wanyama Pori (TANAPA) ,linawashikilia watu wanne akiwemo mmoja ambaye amekamatwa na jino moja na mikia miwili ya Tembo vikiwa na thamani ya Shilingi milioni 60.

WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI KATAVI WATAKIWA KUEPUKA MAZINGIRA YA UKATIRI

Na.Issack Gerald-MPANDA . WANAFUNZI wa Shule za Msingi na Sekondari Mkoani Katavi wametakiwa   kuepuka mazingira yanayopelekea   vitendo ya ukatili na unyanyasaji na   kuzingatia masomo.

WAKALA WA VIPIMO TANZANIA KUZINDUA MATUMIZI YA VIPIMO KESHO MKOANI KATAVI

Na.Issack Gerald-MPANDA Wakala wa vipimo Tanzania Kesho wanatarajia kuzindua na kukopesha mizani kwa wafanyabiashara wadogo Mkoani Katavi kwa ajili ya kuondokana na hasara zinazotokana na kuuza bidhaa mbalimbali pasipo kutumia vipimo halali.