Posts

UNAMFAHAMU MAGUFULI NA MAISHA YAKE TANGU KUZALIWA HADI SIASA?ONGEZA CHAKULACHA UBONGO NA P5 TANZANIA

Image
Mhandisi John Pombe Magufuli JOHN POMBE MAGUFULI Magufuli ni Nani? Lakini je Daktari John Magufuli ni Nani? Mgombea wa urais wa chama cha CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2015 Daktari John Pombe Joseph Magufuli ni mbunge wa jimbo la Chato lililoko mkoa wa Geita na ni waziri wa ujenzi wa Tanzania. Alizaliwa tarehe 29 Oktoba 1959 wilayani Chato Mkoani Kagera. Kielimu, daktari Magufuli ana Stashahada ya elimu ya sayansi akibobea kwenye masomo ya Kemia, Hisabati. Mgombea huyo wa urais ana shahada ya umahiri wa Sayansi na shahada ya uzamivu ya kemia. Aidha daktari Magufuli amewahi kufundisha katika shule ya sekondari Sengerema miaka ya themanini kisha akajiunga na mafunzo ya JKT . Alizaliwa Oktoba 1959 Mhandisi John Pombe Magufuli wakati akijiunga na ccm 1995  Alipohitimu, daktari Magufuli na aliaanza kufanya kazi katika kiwanda cha ‘Nyanza Cooperative Union akiwa Mkemia kabla ya kuondoka hapo na kuwania ubunge. Magufuli alianza mbio za ubunge mwaka 1...

WAKAZI MPANDA WANDELEA KUWA GIZANI UMEME KUKATIKA,VIWANDA VYAKOSA UMEME SHUGHULI ZASIMAMA KWA MWEZI SASA

NA.Issack Gerald TATIZO la kukatika Umeme mara kwa mara Mkoani Katavi   limesababisha kuzorota kwa biashara ya mchele, kutokana na kukwama kwa ukoboaji wa mpunga zao linalotegemewa na wakazi wengi   mkoani Katavi.

MGOGORO WA ARDHI MTAA WA NSEMULWA BADO MBICHI,MKURUGENZI ATOA JIBU BILA SULUHU

NA.Issack Gerald-Katavi Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imesema haijapokea malalamiko ya wakazi wa mtaa wa Nsemulwa kutopimiwa viwanja vyao na kutozwa kiwango kikubwa cha pesa tofauti na kilichopangwa kupitia mikutano.

UHAKIKI MAJINA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MANISPAA YA MPANDA WAKWAMA,MKURUGENZI KUTOA TAARIFA BAADA YA VIFAA KUAWASILISHWA

NA.Issack Gerald-KATAVI ZOEZI la uhakiki wa taarifa katika daftari la kudumu la mpiga kura limeelezwa kuchelewa kuanza katika Manispaa ya Mpanda kutokana na kucheleweshwa kwa vifaa, zikiwemo mashine za BVR.

WAKAZI NSEMULWA KUWASHTAKI MAAFISA ARDHI MANISPAA YA MPANDA KWA WAZIRI WA ARDHI WAKIPINGA USUMBUFU UPIMAJI WA VIWANJA

NA.Issack Gerald-KATAVI WAKAZI wa mtaa wa Nsemulwa Kata ya Nsemulwa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamekusudia kumuita Waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi kutatua migogoro ya ardhi, wakiwatuhumu maafisa ardhi Wilayani Mpanda kushindwa kutatua migogoro hiyo kwa miaka mitatu sasa.

P5 TANZANIA INAKULETEA WASIFU WA WAGOMBEA KITI CHA URAIS WA TANZANIA,TUNAANZA NDANI YA UKAWA,Mh.Edward Lowassa

Image
  Edward Lowassa aliyeshika maikikrofoni na aliyevaa shati jeupe Edward Ngoyai Lowassa Edward Ngoyai Lowassa Mbunge Bunge la Tanzania Jimbo la uchaguzi Monduli ( Arusha ) Tarehe ya kuzaliwa 26 Agosti 1953 Chama CHADEMA (tangu 28/07/15) Tar. ya kuingia bunge tangu 1990 Alirudishwa mwaka 2005 Waziri Mkuu wa Tanzania Alingia ofisini 2005 Alitanguliwa na Frederick Sumaye Dini Mkristo Elimu yake Chuo Kikuu Digrii anazoshika MA (Development Studies) University of Bath (Uing.) Kazi mwanasiasa Edward Ngoyayi Lowassa (amezaliwa 26 Agosti 1953 ) ni mwanasiasa nchini Tanzania . Alichaguliwa kuwa Waziri Mkuu wa kumi wa nchi hiyo tarehe 30 Desemba 2005 akajiuzulu tarehe 7 Februari 2008 kwa kutajwa katika kamati ya bunge ya uchunguzi katika utoaji wa tenda kwa kampuni ya ume...

UKAWA WAMPITISHA RASMI LOWASSA KUGOMBEA URAIS WA TANZANIA

Image
  Edward Lowassa Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema kupitia Ukawa NA MWANDISHI WETU -DAR ES SALAAM Chama cha demokrasia na maendeleo chadema   leo kimemuidhinisha Edward lowasa kuwa mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika   mwezi Oktoba mwaka huu.  Wajumbe wa mkutano mkuu wa chadema uliofanyika   leo Jijini   Dar Es salaam wamepiga kura ya   kuridhia kiongozi huyo aliyejiunga na upinzani akitokea chama tawala CCM kuwa mgombea   Kiti hicho cha   urais   Kupitia chama hicho.  Mwanasiasa huyo Mkongwe hapa Nchini amekuwa   akiyagawa   maoni ya Watanzania tangu akihame chama cha Mapinduzi na Kuhamia chama cha   chadema   tang u vikao vya uteuzi vya ccm   kumpitisha mgombea wa urais kulikata jina lake. Hata hivyo katibu mkuu wa chadema Wilbroad Slaa hakuhudhuria mkutano huo mkuu Kutokana na kuwepo kwa taarifa kuwa hakufurahishwa   na uamuzi wa chadema kumpo...