Posts

MKUU WA MKOA WA KATAVI AFUTURISHA,MAMIA KADA MBALIMBALI ALIOWAARIKA WAHUDHURIA AWAASA KUDUMISHA AMANI

Image
Mkuu wa Mkoa akizungumza na kada mbalimbali aliowaarika kushiriki kwa pamoja katika Ikulu ndogo Mjini Mpanda Mkuu wa Mkoa katikakti wakifuturu Mkuu wa Mkoa wa Katavi wa NNE kutoka kulia katika picha wakiswali  Na.Issack Gerald-Katavi MKUU wa Mkoa wa Katavi Dk. Ibrahim Hamisi Msengi amesisitiza kuwepo kwa amani, upendo na ushirikiano na kusema kuwa  ni fursa nzuri kwa watu kufanya shughuli za maendeleo.

WANANCHI WILAYANI MLELE WATAKIWA KUFICHUA WANAOFANYA VITENDO VYA UKATIRI

Image
Katikati ni mkuu wa Wilaya ya Mlele Issa Njiku akifafanua jambo NA.Issack Gerald-Mlele Wakazi kata ya Kibaoni Wilayani Mlele Mkoani Katavi wametakiwa kushirikiana na vyombo vya dora kutoa taarifa za vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.

WALIMU WAPYA MPANDA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA WELEDI,KUTOJIHUSISHA NA ANASA KAZINI

Image
Walimu wapya wakiwa katika warsha ya pamoja na maafisa elimu mjini Mpanda Na.Amosi Venance-Mpanda Katavi WALIMU wa sekondari wilayani Mpanda mkoani Katavi wametakiwa kuwa na maadili na kufuata weledi katika utendaji kazi ili kuboresha kiwango cha elimu mkoani Katavi.

ZAIDI YA MILIONI TANO ZATUMIKA KUNUNUA VIFAA MAABARA NSIMBO ,WAZAZI WATAKIWA KUTOWAZUIA WATOTO KUSOMA SAYANSI

Image
  Moja ya vyumba vya maabara Shule ya Sekondari Machimboni Na.Issack Gerald -Nsimbo Katavi Wazazi na walezi katika Halmshauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi   wametakiwa kutowazuia watoto wao kupata fursa ya elimu.

KATAVI YATANGAZA VITA DHIDI YA MAUAJI YA WATU WENYE UALBINO TENA

Image
Remi  Luchumi(30) mkazi wa Mwamachoma   Tarafa ya Mamba Wilaya ya Mlele akiwa hospitali ya Wilaya ya Mpanda baada ya kukatwa mkono mwezi juni mwaka huu Na.Issack Gerald-Katavi HALMASHAURI ya wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeweka mikakati ya kukomesha mauaji dhdi ya watu wenye albino.

WAGOMA KUSHIRIKI SHUGHULI ZA MAENDELEO MPAKA WASOMEWE MAPATO NA MATUMIZI

Image
NA.Issack Gerald-Nsimbo Katavi Wakazi wa kijiji cha Magamba kilichopo kata ya Magamba Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi wamesema hawatashiriki shughuli mbalimbali za maendeleo zikiwemo  za ufyatuaji tofali za kijiji ikiwa hawatasomewa taarifa ya mapato na matumizi iliyo sahihi.

MTOTO MIAKA 17 AFA MAJI MPANDA

Image
Na.Issack Gerald-Mpanda Katavi MTOTO aliyefahamika kwa jina la Stanslaus Christopher mwenye umri wa miaka (17) Mkazi wa Mtaa wa Mpadeco Kata ya Makanyagio Wilayani Mpanda Mkoani Katavi, amekufa maji baada ya kutumbukia mtoni katika daraja la Kachoma.