Posts

DC TANGAYIKA AKAZA MWENDO DHIDI YA WAHARIFU

Image
Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi Salehe Mhando amesema,vyombo vya ulinzi na usalama wilayani humo vinaendelea kuwasaka na kuwakamata waharifu mbalimbali wanaohatarisha usalama wa raia na mali zao ili kuwafikisha katika vyombo vya sheria. Muhando ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kuhusu utekelezaji wa agizo lake alilolitoa hivi karibuni akiwataka wanaomiliki silaha kinyume na sheria kuzisalimisha ambapo amesema silaha tatu zimekamatwa. Aidha pamoja na mambo mengine Mhando amewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kupambana na uharifu unaojitokeza huku akiwataka wanaomiliki silaha bila kibali halali kuendelea kuzisalimisha ili kuepuka mkono wa sheria. Wakazi wilayani Tanganyika wanataja miongoni mwa matukio yanayotokea mbali na mauaji kuwa ni uporaji wa mali za raia nyakati za usiku tangu kuanza mwaka 2018. Januari 22 mwaka huu,mkuu wa Wilaya Salehe Mhando akiwa ziarani kata ya Kasekese alitoa agizo kwa wanaomiliki silaha kinyume na sh...

MIKOA 11 YATAHADHARISHWA NA TMA KUHUSU MVUA KUBWA

Image
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),imetoa tahadhari ya vipindi vya mvua kubwa vinavyotarajiwa kuendelea katika maeneo ya mikoa 11 nchini. TMA imetaja mikoa itakayoathirika na mvua hizo ni Dar es Salaam,Pwani,Lindi,Mtwara,Morogoro,Ruvuma,Rukwa, Mbeya,Songwe,Iringa na Njombe. Taarifa iliyotolewa leo na mamlaka hiyo inabainisha kuwa kuanzia leo Machi 12 hadi 13,2018 kunatarajiwa vipindi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24. Taarifa hiyo inaeleza kuwa hali hiyo inatokana na kuendelea kuimarika kwa ukanda wa mvua huku wakazi wa maeneo yaliyotajwa wakitakiwa kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa na tahadhari zinazotolewa. Aidha TMA imesema inaendelea kufuatilia hali hiyo na itatoa mrejesho kila itakapobidi. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

RAIS MAGUFULI ASEMA ANAPATA TABU

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk. John Pombe Magufuli amekiri kupata wakati mgumu katika uteuzi wa Baraza la Mawaziri kutokana na kuwa Mkoa wa Singida kujaa Wabunge wenye sifa zote za kushika nyadhifa hizo . Akiwa katika uzinduzi wa kiwanda cha mafuta ya alizeti mkoani  Singida,Rais Magufuli amesema kwamba anafurahishwa sana na utendaji kazi wa wabunge hao kiasi kwamba alitamani kuwateua wote kuwa katika baraza lake. Rais amesema kwamba Wabunge wa mkoa huo wamekuwa wakimfurahisha katika utendaji kazi wao wa kuwatumikia wananchi. Aidha Rais Magufuli amekiri kufurahishwa na wakazi wa Singida kwani wamekuwa wakitekeleza kauli ya 'Hapa Kazi Tu' kwa vitendo kwa  kulima sehemu kubwa ya mkoa huo ambapo amejionea mwenyewe akiwa katika safari ya gari kuelekea mkoani hapo. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

BARAZA LA WAKUNGA LATOA TAMKO

Image
Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania limelaani na kutoa pole kwa Wauguzi kutokana na matukio yaliyofanywa na viongozi ikiwemo kuwekwa rumande na kupigwa katika mazingira yao ya kazi. Taarifa kutoka katika baraza hilo,iliyotolewa na Lena   Mfalila imesema vitendo hivyo ni udhalilishaji na ni kinyume cha miongozo ya kisheria inayosimamia ushughulikiaji wa tuhuma za uvunjifu wa nidhamu na sheria wakati wa kazi.

RAIS JOHN MAGUFULI ATOA AGIZO KWA WAZIRI WA VIWANDA,BIASHARA NA UWEKEZAJI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt.John Magufuli amemwagiza Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage kuhakikisha wamiliki wa viwanda vya ndani wanaajiri wazawa. Ametoa agizo hilo leo Jumapili Machi 11,2018 wakati akizindua kiwanda cha kufua vyuma cha Kahama Oil Mill mjini Kahama mkoani Shinyanga.

TUNDU LISSU KUFANYIWA UPASUAJI WA GOTI

Image
Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA),Tundu Lissu anatarajiwa kufanyiwa upasuaji mwingine wa goti la kulia Machi 14,2018 katika Hospitali ya Chuo kikuu cha Leuven, Gasthuisberg ili kumnusuru asipatikane na athari za mifupa kutojiunga kwa wakati.

JESHI LA POLISI LAWAZUIA ACT-WAZALENDO KUFANYA MIKUTANO

Image
Jeshi la Polisi wilayani Mvomero Mkoani Morogoro limekitaka chama cha ACT Wazalendo wilayani humo kusitisha kufanya mikutano ya ndani.