Posts

WENYE SIFA YA KUPIGA KURA KATAVI WATAKIWA KUHAKIKI MAJINA YAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

Image
Nembo ya tume ya taifa ya uchaguzi Tanzania Na.Tume ya taifa ya Uchaguzi-KATAVI WANANCHI   Mkoani Katavi wametakiwa Kufika katika Vituo vyao walivyojiandikishia   Katika daftari la Mpiga Kura ili kuhakiki taarifa zao   Katika daftari la hilo. Kwa Mjibu wa Tangazo lililotolewa na Tume ya taifa ya Uchaguzi NEC Zoezi hilo limeanza Augost Mosi mwaka huu ili kutoa fursa kwa wananchi waliojiandiksha Kuhakiki taarifa zao zilizokosewa kabla ya Muda wa Kupiga Kura. Jaji mstaafu Damian Lubuva mwenyekiti wa tume ya taifa ya Uchaguzio Tanzania Pamoja na Mkoa wa Katavi Mikoa mingine inayotakiwa kuanza zoezi hilo ni Rukwa,Njombe,Iringa,Mtwara,Lindi,Dodoma,Singida,Tabora na Kigoma.

JAMII KATAVI,KIGOMA YATAKIWA KUWA NA UTAWALA BORA MATUMIZI YA RASILIMALI

Na.Issack Gerald-Katavi Jamii katika mikoa ya Katavi na Kigoma imetakiwa kutumia sera ya utawala bora kutunza vyanzo vya rasilimali katika mazingira yanayoizunguka kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

BREAKING NEWS

Habari zilizotufikia hivi punde, Chama cha mapinduzi CCM wilaya ya Mpanda mkoani katavi Kupitia katibu wa chama hicho Bi Elizabeth Kasmiri ametangaza matoteo ya kura za maoni katika jimbo la uchaguzi la Mpanda mjini ngazi ya Ubunge ambayo ni kama ifuatavyo 1. Sebastian Kapufi 7,190 2. Galos Mgawe 2,359 3.Gabriel Mnyere 2000 Kufuatia matokeo hayo Sebastian Kapufi ametangazwa rasimi kuwa mgombea kiti cha ubunge kupitia Chama cha CCM mpanda mjini. Katika hatua nyingine Jimbo la Mpanda vijijini wakati matokeo yakiendelea kuhesabiwa,matokeo yaliyotangzwa pia na Bi Elizabeth Kasmiri yanayoonesha  kama ifuatavyo 1.Suleimani Kakoso 5,313 2.Wiliam Makufwe 1,872 3.Abdalah Sumry 1,685 Bado zoezi la kuhesabu kura  katika kata tano zilizobaki linaendela,endelea kuwa nasi kwa undani wa uahabri kadri tunavyoendelea kuzipata kutoka katika vyanzo vyetu vya habari.

WATUMISHI WA UMMA MPANDA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA SIASA WAKATI WA KAZI

Image
Watumishi wa umma wakiwa katika Ukumbi wa shule ya Sekondari St.Mary's Mpanda katika semina iliyoendeshwa na Kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Mpanda Vicenti Kayombo Watumishi mbalimbali katika manispaa ya Mpandaa katika Semian ukumbi wa Shule ya Sekondari St.Mary's Manispaa ya Mpanda katika kikao cha utum,ishi wa umma kikendeshwa Kaimu Mkurugenzi Halmshauri ya Manispaa ya Mpanda Vicenti Kayombo Na. Mark Ngumba-MPANDA WATUMISHI Wa Umma wametakiwa Kutojihusisha na Maswala ya Siasa wakati wa Kazi na badala yake wahakikishe wanatimiza wajibu wao wa  Kuwahudumia wananchi Katika Maeneo yao ya Kazi.

JESHI LA POLISI KATAVI LAWATAKA WANANCHI KUWA MAKINI MITANDAO YA KIJAMII KUHUSU BVR

Na.Mark Ngumba-MPANDA JESHI La polisi Mkoani Katavi limewataka wananchi Kuwa Makini na Ujumbe unaosambazwa  Katika Mitandao  ya Simu kwa Madai ya Kuhakiki taarifa za watu waliojiandikisha Kupiga kura Kwa Kutumia mashine za Kimtandao BVR.

OFISI ZA MFUKO WA BIMA YA AFYA NHIF ZAFUNGULIWA KATAVI

Image
  Na.Issack Gerald-Katavi Wanachama wa Mfuko wa hifadhi ya afya ya jamii NHIF  Mkoani Katavi wanatarajia kunufaika na  huduma hiyo itakayo kuwa ikitolewa Mkoani hapa badala ya Sumbawanga Mkoani Rukwa kama  ilivyokuwa awali.

JARIBIO LA KUUA KWA IMANI ZA USHIRIKINA WATU SITA WASHIKILIWA

 Na.Issack Gerald-Katavi Watu sita wanashikiliwa na jeshi la polisi Mkoani Katavi kwa tuhuma za kutaka kuvamia na kufanya mauaji ya watu wanaodhaniwa kuwa ni wachawi.