RAIS MAGUFULI AOMBOLEZA KIFO CHA JAJI MSTAAFU WA MAHAKAMA YA RUFANI TANZANIA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe.Prof.Ibrahim Hamis Juma kufuatia kifo cha Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe.Robert Kisanga kilichotokea jana. Rais Dkt.John Magufuli Kwa mjibu wa taarifa ambayo imetolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais IKULu Gerson Msigwa Marehemu amefariki jana katika hospitali ya Regency Jijini Dar es Salaam. Katika salamu hizo Mhe.Rais Magufuli amesema Jaji Mstaafu Robert Kisanga atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa alioutoa kwa Taifa wakati wote wa utumishi wake uliojaa umakini,uchapakazi,uzalendo na ushirikiano. Aidha Mhe.Rais Magufuli amewaombea wafiwa wote wawe na moyo wa subira,uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na amemuombea Marehemu Jaji Mstaafu Kisanga apumzishwe mahali pema peponi. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED