Posts

IGP SIRO AKIWA MKOANI KATAVI AMESISITIZA KUCHUKUA HATUA KALI ZA KISHERIA KWA WAHARIFU NCHINI

Image
Na.Issack Gerald Mkuu wa Polisi nchini IGP Simon Sirro akiwa ziarani Mkoani Katavi,amesema Jeshi la polisi litaendelea kuchukua hatua kali za kisheria kwa watu wote wanaojihusisha na uharifu mbalimbali ikiwemo Mauaji ya watu kwa imani za kishirikina. IGP Sirro ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kupokea ripoti ya mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga kuhusu hali ya ulinzi,amani na usalama mkoani Katavi. Aidha Siro amesema uharifu Mkoani Katavi umepungua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na uharifu uliokuwepo katika miaka michache iliyopita. Wakati huo huo Kamanda Sirro ambaye aliwasili jana Mkoani Katavi kwa zaiara ya kikazi ya siku mbili,ameweka jiwe la msingi ujenzi wa zahanati ya jeshi la polisi Mjini Mpanda. Katika hatua nyingine IGP akiwa ameambatana na maafisa wa polisi kutoka makao makuu ya polisi nchini pamoja na waliopo Mkoani Katavi,amekagua na kuangalia maonesho mbalimbali ya namna jeshi la Polisi Mkoani...

SERIKALI IMEAGIZA KUSITISHA UVUVI ZIWA RUKWA

Image
Na.Issack Gerald SERIKALI mkoani  Rukwa imeagiza kulifunga ziwa Rukwa kwa muda usiojulikana kutokana na shughuli za uvuvi kuchangia kasi ya ugonjwa wa kipindupindu katika ziwa hilo. Mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo alitoa agizo hilo wakati akizingumza na wavuvi kwa lengo la kuwaeleza sababu za kulifunga ziwa hilo na kuzuia kabisa uvuvi kutoendelea. Alisema baada ya kukaa na wataalamu wa afya wamekubaliana kusitisha shughuli za uvuvi kwani zimekuwa chanzo kikubwa cha kuenea ugonjwa huo.  Alisema athari inayopatikana katika kambi hizo za uvuvi zitawaathiri walaji wa samaki wanaotokana ziwa hilo hasa waliopo Sumbawanga mjini kwani wanategemea samaki hapo Kama kutoweo na kuwataka walio waliopiga kambi katika ziwa hilo kwa ajili ya uvuvi waondoke mara moja kwani hawataruhusiwa kuingia ziwani kuendelea kuvua samaki.  Wakati huo huo aliagiza kufunguliwa maeneo maalumu kwa ajili ya kuwatibia wagonjwa  watakaopatikana kwani wasipofanya hivyo mlipuko wa ugonjwa huo...

UTAPELI NJE YA IKULU NDOGO MKOANI KATAVI

Image
Na.Issack Gerald Taasisi ya  kupambana na kuzuia  rushwa TAKUKURU  Mkoani  Katavi  imewakamata watu wawili ambao walijifanya kuwa ni maafisa watasisi hiyo na kwenda kupokea rushwa ya shilingi 400,000 karibu na majengo ya ikilu ndogo.  Watuhimiwa hao waliofahamika kwa Majina ya Nicodemo  Peter  pamoja na  Peter   Mwaninsawa  wakazi wa  Mtaa wa  Nsemlwa katika  Manispaa ya  Mpanda walijifanya maafisa wa takukuru na kutapeli fedha hizo. Tukio hilo lilitokea  jana   majira ya saa 4 asubuhi nje ya Ikulu  ndogo ya  Mkoa wa  Katavi  iliyopo  jirani na   ofisi ya TAKUKURU. Mkuu wa  Takukuru mkoani Katavi  John   Minyenya  amewaambia  wandishi wa  habari kuwa watuhumiwa  hao walikamatwa  kufuatia...

RAIS MAGUFULI ATOA AHGIZO LA KIUCHUMI KWA BOT

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli ameitaka Benki Kuu ya Tanzania ( BOT ) kudhibiti matumizi ya fedha za kigeni katika biashara na huduma hapa nchini ili kulinda nguvu ya fedha ya Tanzania na kukabiliana na uhalifu wa kifedha. Mhe.Magufuli ametoa agizo hilo leo wakati akifungua tawi la benki ya CRDB-LAPF Dodoma na kubainisha kuwa hatua hiyo itasaidia kuimarisha uchumi wa nchi. Aidha,Mhe.Rais Magufuli ameitaka BOT kuongeza usimamizi wa benki zinazoendesha shughuli zake hapa nchini ikiwa ni pamoja na kuhakikisha zinajiunga na mfumo wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielektroniki na kufuatilia kwa ukaribu utendaji wake wa kila siku ili ziwe na manufaa kwa nchi. Wakati huo huo Mhe.Rais Magufuli ameipongeza benki ya CRDB kwa kuendeshwa kwa ufanisi tangu ilipobinafsishwa kutoka Serikalini ambapo katika kipindi cha miaka 10 imelipa kodi serikalini kiasi cha Shilingi Bilioni 800,imetoa ajira kwa Watanzania 3,200,imetoa gawio Serikalini la Shilingi Bilio...

UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA MKOANI KATAVI,ZAIDI YA WANAFUNZI 9000 WAMEKOSA NAFASI YA KUIJUNGA KIDATO CHA KWANZA MAWAK 2018

Image
Na.Issack Gerald Zaidi ya wanafunzi 9000 waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mkoani Katavi wamekosa nafasi ya kuingia kidato cha kwanza kwa mwaka 2018 kutokana na upungufu wa vyumba vya madarasa.  Akitangaza matokeo ya mtihani huo katika kikao maalumu cha uchaguzi wa wanafunzi Afisa Elimu mkoa wa Katavi Ernest Hinju amesema jumla watahiniwa 7,190 wamechaguliwa kujiunga na shule za sekondari za kutwa. Aidha watahiniwa 162 hawakuweza kufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali hali iliyopelekea wadau wa elimu kujadili changamoto za kushuka kwa elimu, kwani kulinganisha na mwaka uliopita mkoa wa Katavi umeshika nafasi ya 9 kitaifa kutoka nafasi ya 2 mwaka uliopita  Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Katavi Bw. Gideon Marandu amezitaka halmashauri zote kuhakikisha wanafunzi waliokosa nafasi wanapata nafasi ifikapo Februari mwaka 2018. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

WANAWAKE WAJAWAZITO WILAYANI MPANDA WANALAZIMIKA KUBEBA MAJI KUTOKA NYUMBANI MPAKA ZAHANATI KWA AJILI YA USAFI WAKATI WA KUJIFUNGUA

Na.Issack Gerald Wanawake wote wajawazito katika kijiji cha Mtambo kata ya Katumba Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi, wanalazimika kubeba maji kutoka nyumbani na kuyapeleka katika zahanati ya Mtambo iliyopo kijijini hapo ili yatumike wakati wakijifungua. Mganga mfawidhi wa zahanti hiyo Dkt.Daud Mashama amesema wanawake wajawazito wasi pokuja na maji hulazimika kufuata maji mto Kalutonya uliopo umbali wa kilomita 8 kutoka zahanati ya Mtambo. Kaimu afisa Mtendaji wa kata ya Katumba Bi.Lucy Kagine amekiri kuwepo kwa tatizo la maji katika kijiji cha Mtambo huku akisema mara kwa mara kila wanapochimba visima upatikanaji wa maji umekuwa mgumu. Kwa upande wake Katibu wa kijiji cha Mtambo Bw.Fenias Fulujensi pamoja na mambo mengine amesema wanasubiri uwekaji wa mitambo katika kisima kilichochimbwa ili kusukuma maji. Kwa mjibu wa wakazi wa kijiji cha Mtambo,zahanati ya Mtambo ilijengwa miaka ya 1992 ambapo hata hivyo Juhudi za kutafuta uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya...

MASHEHE 5 MKOANI KATAVI WAMEJIUZURU

Image
Na.Issack Gerald Mashehe watano akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Baraza Kuu la Waislamu (Bakwata) Mkoa wa Katavi, Shehe Shaaban Bakari wamesema kujizulu kwao ni kutokana na shehe wa Mkoa wa Katavi kukiuka Katiba ya Bakwata. Katika picha ni Shehe Mashaka Kakulukulu miongoni mwa waliojiuzuru Wajumbe waliojiuzulu wakiwemo Mashehe Mohamad Shaaban Sigulu na Said Haruna Omary wamemtuhumu Shehe wa Mkoa Ally Hussein kuwa kinara wa kukiuka kat iba ya Bakwata. Wajumbe wengine wa baraza la mashehe Mkoa waliojiuzuru ujumbe ni Shehe Mashaka Nassoro Kakulukulu na Hassan Mbaruku. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bakwata Mkoani Katavi Shehe Shaban Bakari ambaye naye juzi amejiuzuru,amesema Shehe wa Mkoa wa Katavi Ally Hussein amekuwa akizuia maendeleo ya dini ya kiislamu kwa kutokubaliana na maamuzi ya vikao halali huku akiunga mkono waharifu na wanaopinga maendeleo ndani ya dini. Aidha Shehe Bakari amesema sababu nyingine ambayo imewafanya wajiuzuru ni baada ya shehe...