Posts

RAIS MAGUFULI ATOA AHGIZO LA KIUCHUMI KWA BOT

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli ameitaka Benki Kuu ya Tanzania ( BOT ) kudhibiti matumizi ya fedha za kigeni katika biashara na huduma hapa nchini ili kulinda nguvu ya fedha ya Tanzania na kukabiliana na uhalifu wa kifedha. Mhe.Magufuli ametoa agizo hilo leo wakati akifungua tawi la benki ya CRDB-LAPF Dodoma na kubainisha kuwa hatua hiyo itasaidia kuimarisha uchumi wa nchi. Aidha,Mhe.Rais Magufuli ameitaka BOT kuongeza usimamizi wa benki zinazoendesha shughuli zake hapa nchini ikiwa ni pamoja na kuhakikisha zinajiunga na mfumo wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielektroniki na kufuatilia kwa ukaribu utendaji wake wa kila siku ili ziwe na manufaa kwa nchi. Wakati huo huo Mhe.Rais Magufuli ameipongeza benki ya CRDB kwa kuendeshwa kwa ufanisi tangu ilipobinafsishwa kutoka Serikalini ambapo katika kipindi cha miaka 10 imelipa kodi serikalini kiasi cha Shilingi Bilioni 800,imetoa ajira kwa Watanzania 3,200,imetoa gawio Serikalini la Shilingi Bilio...

UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA MKOANI KATAVI,ZAIDI YA WANAFUNZI 9000 WAMEKOSA NAFASI YA KUIJUNGA KIDATO CHA KWANZA MAWAK 2018

Image
Na.Issack Gerald Zaidi ya wanafunzi 9000 waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mkoani Katavi wamekosa nafasi ya kuingia kidato cha kwanza kwa mwaka 2018 kutokana na upungufu wa vyumba vya madarasa.  Akitangaza matokeo ya mtihani huo katika kikao maalumu cha uchaguzi wa wanafunzi Afisa Elimu mkoa wa Katavi Ernest Hinju amesema jumla watahiniwa 7,190 wamechaguliwa kujiunga na shule za sekondari za kutwa. Aidha watahiniwa 162 hawakuweza kufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali hali iliyopelekea wadau wa elimu kujadili changamoto za kushuka kwa elimu, kwani kulinganisha na mwaka uliopita mkoa wa Katavi umeshika nafasi ya 9 kitaifa kutoka nafasi ya 2 mwaka uliopita  Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Katavi Bw. Gideon Marandu amezitaka halmashauri zote kuhakikisha wanafunzi waliokosa nafasi wanapata nafasi ifikapo Februari mwaka 2018. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

WANAWAKE WAJAWAZITO WILAYANI MPANDA WANALAZIMIKA KUBEBA MAJI KUTOKA NYUMBANI MPAKA ZAHANATI KWA AJILI YA USAFI WAKATI WA KUJIFUNGUA

Na.Issack Gerald Wanawake wote wajawazito katika kijiji cha Mtambo kata ya Katumba Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi, wanalazimika kubeba maji kutoka nyumbani na kuyapeleka katika zahanati ya Mtambo iliyopo kijijini hapo ili yatumike wakati wakijifungua. Mganga mfawidhi wa zahanti hiyo Dkt.Daud Mashama amesema wanawake wajawazito wasi pokuja na maji hulazimika kufuata maji mto Kalutonya uliopo umbali wa kilomita 8 kutoka zahanati ya Mtambo. Kaimu afisa Mtendaji wa kata ya Katumba Bi.Lucy Kagine amekiri kuwepo kwa tatizo la maji katika kijiji cha Mtambo huku akisema mara kwa mara kila wanapochimba visima upatikanaji wa maji umekuwa mgumu. Kwa upande wake Katibu wa kijiji cha Mtambo Bw.Fenias Fulujensi pamoja na mambo mengine amesema wanasubiri uwekaji wa mitambo katika kisima kilichochimbwa ili kusukuma maji. Kwa mjibu wa wakazi wa kijiji cha Mtambo,zahanati ya Mtambo ilijengwa miaka ya 1992 ambapo hata hivyo Juhudi za kutafuta uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya...

MASHEHE 5 MKOANI KATAVI WAMEJIUZURU

Image
Na.Issack Gerald Mashehe watano akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Baraza Kuu la Waislamu (Bakwata) Mkoa wa Katavi, Shehe Shaaban Bakari wamesema kujizulu kwao ni kutokana na shehe wa Mkoa wa Katavi kukiuka Katiba ya Bakwata. Katika picha ni Shehe Mashaka Kakulukulu miongoni mwa waliojiuzuru Wajumbe waliojiuzulu wakiwemo Mashehe Mohamad Shaaban Sigulu na Said Haruna Omary wamemtuhumu Shehe wa Mkoa Ally Hussein kuwa kinara wa kukiuka kat iba ya Bakwata. Wajumbe wengine wa baraza la mashehe Mkoa waliojiuzuru ujumbe ni Shehe Mashaka Nassoro Kakulukulu na Hassan Mbaruku. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bakwata Mkoani Katavi Shehe Shaban Bakari ambaye naye juzi amejiuzuru,amesema Shehe wa Mkoa wa Katavi Ally Hussein amekuwa akizuia maendeleo ya dini ya kiislamu kwa kutokubaliana na maamuzi ya vikao halali huku akiunga mkono waharifu na wanaopinga maendeleo ndani ya dini. Aidha Shehe Bakari amesema sababu nyingine ambayo imewafanya wajiuzuru ni baada ya shehe...

TAAS MKOANI KATAVI WAMEKATAA KUITWA WALEMAVU WA NGOZI

Image
Na.Issack Gerald Chama cha watu wenye Ualbino Tanzania (TAAS) Mkoani Katavi kimewataka watanzania kutowaita wao kama watu wenye ulemavu wa ngozi albino badala yake wawaite watu wenye Ualbino. Mwenyekiti wa TAAS Mkoani Katavi Victus Kweka Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa chama hicho Mkoani Katavi Bw.Victus Kweka kupitia kikao cha kujadili kupinga ukatiri,unyanyasaji na ukandamizaji wa haki za w atu wenye ulemavu kwa kuwanyima haki za msingi kama elimu,afya na haki nyingine za kibinadamu. Amesema rangi ya ngozi waliyonayo watu wenye ualbino siyo ulemavu wa ngozi bali wao wanahesabika katika kundi la watu wenye ulemavu wa macho kutokana hali waliyonayo. Kwa upande wake mratibu wa wa elimu jumuishi Wilayani Mpanda Bi.Ashura Shabaani ambaye pia ni msichana mwenye ualbino amesema mpaka sasa bado kuna baadhi ya watu wenye ualbino wanaojinyanyapaa. Amewataka watu wenye ualbino kuchanganyikana na jamii ili kupata elimu inayowawezesha kufahamu haki zao,kupatiwa mafuta ya kupu...

WAZIRI WA MAJI NAYE AMTUMBUA MHANDISI WA MAJI MKOANI RUKWA

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe amemsimamisha kazi Mhandisi Goyagoya Mbena kwa tuhuma za kusaini barua ya kuruhusu ujenzi wa mradi wa Maji wilayani Nkasi mkoani Rukwa. Taarifa ambayo imetolewa jana na Wizara hiyo,imeeleza kuwa Mhandisi Mbena amesaini barua kwa niaba ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo kinyume cha utaratibu. Mradi huo wa Maji katika kijiji cha Kamwanda Halmashauri ya Nkasi mkoani Rukwa u meelezwa kuwa na thamani ya shilingi bilioni 7.4. Siku ya Juzi Waziri wan chi ofisi ya Rais tawala za Mikoa na serikali za mitaa Mh.Suleiman Jafo,alimsimamisha kazi Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa Julius Kawondo kwa tuhuma za kujihusisha na rushwa na matumizi mabaya yaliyoisababishia Serikali hasara ya Sh 7 bilioni. Chanzo:eatv Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

MVUA YA LEO MKOANI KATAVI IMELETA MADHARA

Na.Issack Gerald Mvua zinazoendelea kunyesha mkoani Katavi zimesababisha madhara katika makazi ya wakazi wa Mtaa wa Misunkumilo uliopo Manispaa ya Mpanda ukiwemo uharibifu wa miundombinu. Baadhi ya wananchi ambao makazi yao yameharibiwa ikiwemo kufa kwa mifugo kutokana na maji kukosa mwelekeo hali inayosababishwa na kutokuwepo kwa mitaro ya maji wameiomba serikali ichukue hatua. Kwa upande wa Mwenyekiti wa mtaa huo BW Katabi Jona ameutaka uongozi wa Manispaa kuichukulia hatua Kandarasi iliyo husika na ujenzi wa barabara za mtaa huo bila kuweka mitaro. Haya yana jili ikiwa ni siku moja tu tangu mamlaka ya hali ya hewa nchini TMA kutoa tahadhari juu ya uwepo wa Mvua kubwa. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED