Posts

SHULE YA MSINGI NSAMBWE YAKABILIWA NA UPUNGUFU VYUMBA VYA MADARASA-Agosti 3,2017

Zaidi ya wanafunzi 250 wa shule ya msingi Nsambwe iliyopo kata ya Misunkumilo Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda wanalazimika kusomea nnje k utokana na upungufu wa vyumba vya madarasa.

WILAYA YA MLELE YAZINDUA MKAKATI WA MAENDELEO WA MIAKA MITANO-Agosti 3,2017

Halmashauri ya wilaya ya Mlele mkoani Katavi imezindua mpango mkakati wa miaka mitano wa maendeleo ya mwaka 2016/2017 hadi mwaka 2021.

WAHAMIAJI HARAMU WILAYANI MLELE MKOANI KATAVI KUANZA KUSAKWA-Agosti 2,2017

Mkuu wa wilaya ya mlele mkoani Katavi Rahel Kasanda amewaagiza watendaji wa idara mbalimbali kataka Halmashauri hiyo kushirikiana vema na wananchi katika kuwabaini wahamiaji haramu wanaoingia katika wilaya hiyo. 

WAKAZI MANISPAA YA MPANDA WAUNGA MKONO DAWA ZA CHANJO KWA WATOTO ZICHUNGUZWE KUTOKANA NA WATOTO KULEWA,KUANGUKA NA KUZIMIA WANAPOTUMIA DAWA HIZO-Agosti 2,2017

Baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,wameunga mkono hoja ya baadhi ya madiwani waliotaka ziangaliwe upya dawa za chanjo zinazosababisha wanafunzi wa shule za msingi kuanguka na kuzimia baada ya kunywa dawa hizo.

WIKI YA UNYONYESHAJI DUNIANI YAANZA,WAZAZI KATAVI WAASWA KUNYONYESHA KWA MUDA WA KUTOSHA KWA AJILI YA AFYA ZA WATOTO-Agosti 2,2017

Ikiwa ni wiki ya unyonyeshaji duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo mwezi wa nane,wazazi  mkoani Katavi  wametakiwa kuwanyonyesha watoto mpaka wafikiapo umri wa miaka miwili ili kulinda afya zao.  Muuguzi wa kituo cha afya cha Town Clinic katika halmashauri ya  Manispaa ya Mpanda Mkoani  Katavi Lugalata Elias amesema  ikiwa ni wiki ya unyonyeshaji maziwa,  wazazi wanatakiwa kufuata ushauri wanaopewa na watoa  huduma ili kuepuka kudhoofika kwa afya ya mtoto.

DC MPANDA ATAKA VIONGOZI NGAZI ZOTE KUSHIKAMANA PAMOJA KUSUKUMA GURUDUMU LA MAENDELEO-Julai 31,2017

MKUU wa Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi Bi.Lilian Matinga,amewataka viongozi wote wilayani Mpanda kushikamana kwa pamoja katika kusukuma maendeleo ya Mkoa wa Katavi.

WAKAZI WILAYANI MPANDA WALALAMIKIA SERIKALI KUHUSU SHIRIKA LA MAENDELEO YA PETROLI TANZANIA (TPDC) KUTUNZA KICHAKA MTAA WA MSASANI KWA MIAKA 25 BILA KUENDELEZA MRADI NA HATIMAYE KICHAKA HICHO KIMEGEUKA KUWA MAFICHO YA VIBAKA NA WEZI-Julai 31,2017

WAKAZI wa Mtaa wa Masasani Wilayani Mpanda Mkoani Katavi,wamelalamikia hatua ya eneo la uwekezaji wa shirika la maendeleo ya Petrol Tanzania TPDC kuwa maficho ya uharifu kutokana na eneo hilo kuwa kichaka baada ya kutoendelezwa kwa zaidi ya miaka 25 sasa.