MGOGORO WA ARDHI KIJIJI CHA TUMAINI WILAYANI MPANDA WATOKOTA



Na.Issack Gerald Bathromeo-Mpanda
Serikali ya kijiji cha Tumaini Halmshauri ya Wilaya ya Nsimbo Wilayani Mpanda mkoani Katavi,imewalalamikia watu wanaowatishia maisha kwa madai kuwa kijiji hicho kinataka kuwanyang’anya ardhi yao.
Viongozi wa serikali ya kijiji cha Tumaini katika picha ya pamoja,wa tatu kutoka kushoto ni mwenyekiti wa kijiji Bw.Billu Bukwaya na wakwanza kutoka kushoto(mwenye shati nyeupe) ni  mwenyekiti wa kitongoji cha Tulieni na wengine waliobaki ni wajumbe wa kamati ya ardhi ya Kijiji cha Tumaini(PICHA NA.Issack Gerald)

Uongozi wa kijiji hicho umesema kuwa,vitisho vya maisha wanavipata kutoka kwa baadhi ya viongozi waliokuwepo madarakani katika kipindi cha uongozi uliopita ambapo takribani watu 10 wakiwemo viongozi hao ndio wanadaiwa kuhodhi heka 2850 bila kufuata utaratibu wa sheria za kijiji.
Kwa mjibu wa taarifa ya Muhtasari wa kikao cha Halmsahuri ya Kijiji cha Tumaini kilichofanyika Aprili 16 mwaka huu,inaonesha kuiwa miongoni mwa wanaotuhumiwa kuhodhi ardhi kwa kukiuka kifungu cha 8 cha sheria ya ardhi ya kijiji namba ‘5’ ya mwaka 1999 ni Bw.Willium Midende mwenyekiti wa zamani wa kijiji cha Tumaini anayedaiwa kuhodhi eneo la Heka 1500,Mwenyekiti wa zamani wa Huduma za Jamii Bw.Kadumi Shija aliyehodhi eneo la heka 200 huku Bw.Mashaka John Malale aliyekuwa katibu wa huduma za jamii kipindi cha uongozi uliopita yeye kwa upande wake akituhumiwa kukimbia na nyaraka za serikali ya kijiji na kuendelea kugawa ardhi kwa kutumia nyaraka hizo.
Hata hivyo watuhumiwa hao walikana tuhuma dhidi yao ikiwemo kuwatishia maisha viongozi wa kijiji cha tumaini ambapo mwenyekiti mstaafu Bw. Willium Midende amsema kuwa eneo analomiliki ni ni kati ya heka 30-35 alizogawiwa na kijiji kihalali huku Bw.Kadumi shija yeye akisema kuwa anamiliki Heka kati ya 25-35 alizopewa na kijjiji ambapo hata hivyo kwa upande wake Bw.Mashaka John Malale aliyekuwa katibu wa huduma za jamii akikanusha kukimbia na nyaraka za serikali na kuzitumia kugawa mashamba ambapo alisema kuwa alizonazo ni taarifa zilizokataliwa katia mkutano wa kijiji pekee.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Kata ya Itenka Bw.Omary Hussein ambaye ametajwa kutopeleka muhtasari katika ngazi ya Halmashauri ya wilaya kwa utatuzi wa migogoro amesema hajakataa kupeleka bali anasubiri muhtasari wa kikao cha Halmshauri ya kijiji cha Tumaini.
Aidha Afisa Mtendaji wa Kata ya Itenka Bw.Omary Hussein amesema,leo amepokea majina manne ya watu wanaodaiwa kuwatishia maisha viongozi wa kijiji cha Tumaini na kuahidi kulishughulikia kwa mjibu wa sheria.
Hata hivyo mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Nsimbo Mh.Raphael Kalinga amesema yeye kama mwenyekiti wa halmshauri ya Wilaya hajapokea taarifa ya mgogoro huo na ametoa wito kwa viongozi wa kijiji cha Tumaini kupeleka taarifa za mgogoro huo ikiwa kuna tatizo ili lishughulikiwe haraka.
Mhariri:Issack Gerald Bathromeo Mashama
Endelea kuhabarika na ‘’P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM’’

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA