Posts

KWA MWAKA 2017 WAPO WENGI WALIOTUMBULIWA NA RAIS MAGUFULI,HAWA NI BAADHI YA VIGOGO

Image
Katika mwaka 2017, mambo mengi yametokea ambayo yametikisa nchi kuanzia kwenye nyanja ya kijamii, kiuchumi, kisiasa na hata kiutamaduni. Imekuwepo mijadala mikubwa sana kuanzia kwenye ajali za barabarani, uchumi wa nchi, utawala, na mambo mengine yanayogusa maisha ya wananchi. Rais Dkt John Magufuli Wakati zikiwa zimesalia siku 6 mwaka 2017 kuisha, na mjadala sasa ukiwa ni sikukuu za Christmas na Mwaka Mpya na suala la Wachagga kurudi makwao, tutakuwa hatujautendea haki kama, japo kwa ufupi hatutakumbushana masuala yaliyotokea kwenye siasa kwa mwaka huu. Mwaka huu, neno “Kutumbua” lilishika kasi sana. Hii ni kutokana na Rais Magufuli ambaye alisema amejipa kazi ya kutumbua majipu, kuwafuta kazi viongozi ambao kwake yeye aliona hawaendani na kasi yake au kutokana na sababu nyingine yoyote. Idadi ya waliotumbuliwa ni wengi, na katika mjadala wetu wa leo, tutaangazia vigogo 12 waliotumbuliwa tangu Januari 1, 2017. 1.  Mhandisi Felchesmi Mramba. Januari Mosi 2017, R...

SERIKALI KUANZA KUWASHGHULIKIA WANAOVAA NUSU UCHI

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni, sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe amesema wizara imeanza kutekeleza agizo la Rais Magufuli juu ya baadhi ya wasanii ambao wanadaiwa kuwa chanzo cha kuporomoka kwa maadili ya kitanzania. Waziri Harison Mwakyembe Waziri Mwakyembe ametoa taarifa hiyo alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari na kusema kwamba kitendo cha Rasi Magufuli kusema suala hilo, kimewapa nguvu ya kuzidi kupambana na wasanii, ambapo hapo awali walikuwa wakiwagusa huwajia juu na kulalamika. Hivi karibuni Rais Magufuli alizitaka mamlaka husika kuwachukulia hatua wasanii wanaovaa nusu utupu kwenye kazi zao za sanaa ambazo zingine huonyeshwa kwenye television, ambazo amedai hazina maadili na zinadhalilisha utamaduni wetu na kuharibu kizazi kijacho. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

NYUMBA YA RAIS KABILA KUCHOMWA MOTO HII NI HATARI NA NUSU

Image
Nyumba ya Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila imechomwa moto katika shambulizi linaloshukiwa kufanywa na waasi, ambapo askari mmoja aliuwa. Rais Joseph Kabila wa Congo DRC Tukio hilo limetokea Desemba 25, 2017, ambapo taarifa zinasema kuwa waasi wa kundi lijulikanalo Mai Mai walijaribu kuiba mali kutoka makazi hayo ya rais yaliyoko eneo la Musienene, katika jimbo la Kivu ya Kaskazini. Wakati wa tukio Rais Kabila hakuwa kwenye nyumba hiyo ambayo iko kijijini maili 1,680 Mashariki mwa mji wa Kinshasa, huku kundi la Mai Mai na kundi la waasi wa ADF wakiwa washukiwa wa kwanza juu ya tukio hilo. Hivi karibuni Rais Kabila amekuwa akipingwa na wanasiasa mbali mbali kwa kitendo chake cha kutaka kugombea nafasi ya urais kwa muhula mwingine. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

BUNDI GANI AMEENDELEA KUTANDA KUHUSIANA NA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS?TUMEPOROMOKA TENA VIWANGO VYA FIFA MPAKA NAFASI YA 147 KUTOKA 142

Image
Taifa Stars Tanzania imezidi kudidimia katika viwango vya soka duniani baada ya kushuka kwa nafasi 5 zaidi kwenye viwango vya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kwa mwezi Novemba. Kupitia taarifa iliyotolewa ljana na Shirikisho la soka duniani FIFA inaonyesha Tanzania inashika nafasi ya 147 kutoka  142 mwezi Oktoba ikiwa imeporomoka kwa nafasi tano kutoka juu. Kwa Uganda wa Afrika Mashariki na Kati,Uganda imeendelea kuongoza ikiwa inashika nafasi ya 75 duniani huku Senegal ikiwa inaongoza kwa Afrika nzima ikiwa inashika nafasi ya 23 kwenye viwango hivyo vya FIFA. Kwa upande wa 10 bora,Ujerumani imeendelea kuongoza ikifuatiwa na Brazil,Ureno,Argentina,Ubelgiji,Hispania,Poland, Uswisi,Ufaransa na Chile. Tanzania ilifanya vibaya kwenye michuano ya CECAFA nchini Kenya mapema mwezi huu pia kwa mwezi Novemba ilipata sare ya 1-1 dhidi ya Benin. Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED